Habari za Punde

 
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akiwasili katika viwanja vya hoteli ya Sea Cliff kuzungumza na Wananchi na Viongozi wa UWT Wilaya ya Kaskazini B Unguja akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Ndh Vuai Mwinyi.  
Mwanafunzi akisoma Quran kabla ya kuaza kwa mkutano huo na Viongozi na Wananchi wa Wilaya ya Kaskazini B Unguja uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya sea cliff mangapwani Zanzibar. 
Katibu wa UWT Wilaya ya Kaskazini B Unguja akisoma risala ya Wananchi wa Wilaya hiyo wakati wa mkutano wao na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, kuzungumza na viongozi hao na wananchi wa wilaya hiyo katika ukumbi wa hoteli ya sea cliff mangapwani Zanzibar.

Mjumbe wa Umoja wa Wake wa Wawakilishi na Wabunge wa CCM Bi Mvita Kibendera akizungumza wakati wa mkutano huo na wananchi Wilaya ya Kaskazini B Unguja. 
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe Vuai Mwinyi akizungumza na kuwasalimia Viongozi na Wananchi wa Wilaya ya Kaskazini B Unguja wakati wa mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya sea cliff mangapwani Zanzibar.








No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.