Na.Haji. Nassor - Pemba.
Kauli
hiyi imetolewa na waziri wa wizara hiyo, Mohammed Bin – Hamel Al Ruhim wakati
alipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya kumaliza ziara
yake ya kutwa moja kisiwani Pemba.
Alisema
tayari ameshafanya mazungumzo na waziri wa
wizara ya Habari ya Zanzibar juu ya azma, kwa watendaji wake wakiwemo
waandishi kupewa taaluma ya utafutaji na uchimbaji wa gesi, ili wawe wajuzi wa
kuwafahamisha kupitia vyombo vya habari.
Alisema
ingawa utafutaji na uchimbaji wa mafuta, taaluma yake inatofautiana kutoka
sehemu moja na nyengine, lakini kama waandishi wa habari na watendaji wengine
wa wizara ya Habari hapa Zanzibar, wakikubaliana watakwenda nchini Oman
kujifunza.
“Niwaambie
waandishi wa habari, hata juzi nimeshafanya mazungumzo na waziri wenu wa habari,
juu ya jambo hili la waandishi kupatiwa taaluma nchini Oman, sasa wacha tuone
maana sisi tunachimba mafuta nchi kavu na huwenda kwa Zanzibar mkayatafuta
baharini”,alisema.
Akizungumzia
kuhusu harakati hizo za uchimbaji wa mafuta wa gesi alisema, Oman imekuwa
ikizungumza na makampuni kadhaa juu ya hilo kwa Zanzibar.
Alisema
ijapokuwa makampuni hayo yamekuwa yakiwaeleza kwenda visiwa Zanzibar kwa ajili
ya utafiti huo, lakini hawana taarifa za wapi wamefikia.
“Tunasoma
sana kwenye vyombo vya habari kama magazeti, lakini hawajatueleza kitu hasa
wamefanya juu ya utafutaji wa uchimbaji wa mafuta na gesi kwa Zanzibar, na hata
Tanzania yote”,alisema.
Kuhusu
sekta ya utalii, alisema amevutiwa na ukarimu na bashasha ya wananchi wa
Zanzibar, maana hilo ni sehemu ya kuvutio cha watalii, jambo ambalo nchi
nyengine hakuna.
Alisema
kutokana na hali ya amani na utulivu alioushuhudia kisiwani Pemba, anajipanga
ili kuhakikisha anarudi tena kisiwani humo, ili atembee zaidi.
Mapema
Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mwanajuma Majid Abdalla, aliushukuru ujumbe huyo
wa serikali ya Oman ukiongozwa na waziri wake wa Mafuta na Gesi.
Alisema
ujio wao kisiwani Pemba, ni ishara ya kuendeleza udugu wa kweli uliopo miongoni
mwa nchi hizo, ambao uliasisiwa na viongozi wa nchi mbili hizo.
Waziri huyo wa mafuta akiambatana na balozi mdogo wa Oman nchini, waziri wa habari, wakiwa na mwenyeji wao Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba, ulitembelea hospitali ya Abdulla mzee, Skuli ya Uweleni, bandarini Mkoani, kiwanda cha makonyo na msitu wa hifadhi wa Ngezi wilaya ya Micheweni
No comments:
Post a Comment