Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, afanya Uteuzi

                            TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, leo amefanya uteuzi wa viongozi katika taasisi mbalimbali za serikali kama ifuatavyo:-

1.   Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu cha 7(1) cha Sheria ya Baraza la Michezo Namba 5 ya 2010, Rais Mheshimiwa Dkt. Shein amemteua Bwana Gulam Abdulla Rashid kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Michezo, Zanzibar.

2.   Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu cha 7(2) cha Sheria ya Mamlaka ya Usafiri Baharini Namba 3 ya mwaka 2009, Rais Dkt. Shein amemteua Meja Jenerali Mstaafu Said S. Omar kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usafiri Baharini.

3.   Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu cha 5 (2) cha Sheria ya KMKM Namba 1 ya 2003, Mheshmiwa Rais Dkt. Shein amemteua Kapteni Khamis Simba Khamis kuwa Naibu Mkuu wa Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM).

4.   Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu cha 12 (1) cha Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Namba 3 ya 2015, Rais Dkt. Shein amemteua Ndugu Farhat Ali Mbarouk kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira katika Wizara ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira.

5.   Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu cha 5(1) cha Sheria ya Shirika la Nyumba Namba 6 ya 2014, Mheshmiwa Rais amemteua Ndugu Riziki Jecha Salim kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba katika Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji.

    Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu 15(1) cha Sheria ya Tawala za Mikoa Namba 8 ya 2014, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein amemteua Ndugu Mkufu Faki Ali kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Wete, Pemba.


Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu iliyosainiwa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dkt  Abdulhamid Yahya Mzee, uteuzi huo unaanzia leo tarehe 17 Oktoba, 2017.     

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.