Habari za Punde

Wakunga na Wauguzi Zanzibar Watembelea Kituo cha Watoto Yatima Nyumba ya Serikali Mazizini na Kukabidhi Misaada ya Vyakula leo.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wakunga na Wauguzi Zanzibar.Bi. Valeria Rashid Haroub akikabidhi Msaada wa Vyakula kwa Afisa wa Ustawi wa Jamii Zanzibar Kitengo cha Watoto Yatima Mazizini Ndg. Juma Makame Kombo,wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa Vyakula na kutoka huduma za kuwapima Afya zao walipowatembelea na kukabidhi msaada huo.








Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wakunga na Wauguzi Zanzibar.Bi. Valeria Rashid Haroub akiwa katika picha ya pamoja na Watoto Wanaoishi katika Nyumba ya Watoto Yatima Mazizini Zanzibar baada ya hafla ya kukabidhi msaada wa Vyakula na kuwapima Afya Zao.(Picha na Abdalla Omar Maelezo – Zanzibar).

Na Mwashungi Tahir-Maelezo Zanzibar.
BARAZA la Wakunga na Wauguzi imefanya ziara ya kuwatembelea watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha Watoto Mazizini Zanzibar kujua maendeleo yao kiafya pamoja na kutowa huduma mbalimbali za kuchunguza Afya zao.
Aidha, katika ziara hiyo, wauguzi waliwapima afya, uzito ili kufahamu kama wanakabiliwa na maradhi mbalimbali, pamoja na kutoa tiba.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa baraza hilo Bi.Valeria Rashid Haroub,  alisema ziara hiyo ni miongoni mwa shughuli mbali mbali zinazofanyikakuelekea siku ya wakunga duniani, ambayo itafikia kilele chake Mei 5, 2018.
Amesema watoto ni viumbe wanaohitaji huduma na uangalizi wa mara kwa mara ili kutambua afya zao, akieleza kuwa, hatua ya kuwapima maradhi ikiwemo kisukari na kujua viwango vyao vya damu, inarahisisha kuwaanzishia tiba mapema kabla hali zao hazijawa mbaya.
“Mtoto ni tegemeo la jamii kwa siku za baadae. Anahitaji huduma zote muhimu ikiwemo malazi,elimu, afya na ishe bora kama alivyomalengoyaserikali,”alisemaMwenyekitihuyo.
Nae Msaidizi mrajisBaraza la wauguzi Rajab KhamisRajab alisema watoto ni muhimu hivyo wanahitaji kupewa huduma zote za jamii.
AkizungumziamaadhimishoyasikuyaWakunganaWauguzi, Valeria alisema baraza hilo limepanga kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo kutembelea maskulini kwa ajili ya kutoa elimu kwa wanafunzi juu ya kujikinga na maradhi tafauti hasa ya mripuko katika kipindi hichi cha mvua.
Aidha, alisema wamejipanga kutoa elimu ya uzazi wa mpango katika vituo mbalimbali mijini na vijijini na kuwashajiisha akinamama kujifungulia hospitali ilikupunguza matatizo yanayoweza kujitokeza wakati wa kujifungua.
Serikaliimewekavituovyaafyavinavyotoahudumaza mama namtotokilasehemuilikuwarahisishiauzazisalama,” alisema Valeria.
Alizitaja miongoni mwa hospitali zitakazotolewa huduma hizo pamoja na elimu kuwa ni Makunduchi Mkoa wa Kusini na Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Hatahivyo, aliwatalawakunganawauguziwasikaevituonikusubiriwananchiwanaofuatahuduma, bali wapite nyumba kwa nyumba kutoa elimu ya afya, uzazi wa mpango pamoja na maradhi mengine.
Katikaziarahiyo, wakunganawauguzihaowalitoazawadikadhaazakwawatoto,ikiwemobiskuti, maziwa, madaftarinanyenginezo.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni wakunga huongeza njia katika utoaji wa huduma bora.”

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.