Habari za Punde

Barack Obama aondoka Tanzania baada ya mapumziko Serengeti, atua Kenya na kukutana na Uhuru Kenyatta na Raila Odinga

Rais Mstaafu wa Marekani Bw Obama akisalimiana na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta baada ya kuwasili Ikulu Nairobi na Naibu Rais William Ruto katika ikulu ya Nairobi.
Bw Obama (kati), dada yake Bi Auma Obama na Rais Kenyatta baada ya rais huyo wa zamani wa Marekani kuwasili Nairobi
Bw Obama na Bw Kenyatta wakitembea ikulu, Nairobi. Nyuma yao ni Bi Auma Obama

Rais Mstaaf wa Marekani Bwana. Obama akisalimiana na Bwana Raila Odinga, alipowasili  Nchini Kenya.

 Hii ni ziara ya nne ya Obama nchini Kenya.
Babake alizaliwa katika eneo la Kogelo mjini Siaya.
Waandalizi wa hafla hiyo wamedai ukosefu wa eneo kubwa la kufanyia sherehe hiyo Siaya kuwa sababu kuu ya raia wengi kutoruhusiwa kuhudhuria uzinduzi huo.
''Kutokana na udogo wa eneo, hafla hiyo itahudhuriwa na watu wachache huku vyombo vichache vya habari pia vikiruhusiwa'', ilisema taarifa ya waandalizi,
Mjini Kisumu skrini kubwa zitawekwa katika uwanja wa michezo wa Jomo Kenyatta ili umma kufuatilia ziara hiyo ya Obama.
Siku ya Jumatatu Obama anatarajiwa kuelekea Kisumu ambapo atapokewa na Gavana wa mji huo Anyang' Nyong'o kabla ya kuelekea Siaya.
Atakapowasili mjini Siaya rais huyo wa zamani wa Marekani atapokewa na Gavana wa Siaya Cornel Rasanga kabla ya kusafirishwa hadi katika kijiji cha Kogelo ambako familia yake ya kenya inatoka ili kuzindua wakfu huo wa Sauti Kuu.
Wawakilishi , wasomi, viongozi wa dini na viongozi wa kijiji walikutana mjini Kogelo siku ya Ijumaa katika kile kiongozi wao alisema kwamba wanajadiliana jinsi ya kumkaribisha bwana Obama.
"Tulikuwa tukijadiliana kuhusu tutakavyomkaribisha. Pia tumejadiliana kuhusu mahitaji ya jamii ambayo tutataka kuwasilisha kwa Obama siku ya Jumatatu, Nicholas Rajula aliambia gazei la Daily Nation nchini Kenya.
''Tunataka kumkaribisha katika kijiji kwa njia ya Kiafrika. Hii itafanyika iwapo kutakuwa na raia wengi. Kwa sababu hiyo tunataka kutoa ombi kwa waandalizi kumruhusu mwana wetu kuhutubia umma kwa ufupi, sio lazima katika eneo la hafla hiyo kwa kuwa ni dogo mno kuruhusu kila mtu kuingia.
Baada ya ziara yake nchini Kenya Obama ataelekea Afrika Kusini.Hii itakuwa ziara yake ya kwanza nchini Kenya tangu kuondoka madarakani mnamo mwezi Januari 20 mwaka 2017.
Amezuri nchini Kenya mara tatu 1987, 1992 na 2015 wakati alipokuwa akihudumu kwa awamu ya pili ya urais.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.