Rais Dk. Shein alikutana na uongozi wa Ofisi ya
Rais Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, chini ya Waziri wake
Haroun Ali Suleiman ambaye katika maelezo yake ya utangulizi alieleza
vipaumbele vilivyowekwa na Ofisi hiyo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa jengo jipya
la Mahkama Kuu Tunguu na jingo la Ofisi ya Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu
wa Uchumi.
Kipaumbele chengine alieleza kuwa ni pamoja na
kuwezesha shughuli za Serikali na utoaji wa huduma kufanyika kielektroniki,
kuendelea kutayarisha miongozo mbali mbali ya Utumishi wa Umma na kusimamia
utekelezaji wake, kutekeleza program ya Mabadiliko katika Sekta ya Sheria na
Mabadiliko ya Utumishi wa Umma pamoja na
kuimarisha usimamizi wa misingi ya Utawala Bora.
Nae Rais Dk. Shein wka upande wake aliupongeza
uongozi wa Ofisi hiyo kwa kuendelea kutekeleza vyema kazi zake pamoja na
kuwasilisha vyema utekelezaji wa Mpango Kazi kwa Ofisi hiyo.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment