Habari za Punde

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Aondoka Nchini Namibia Baada ya Kumalizika Kwa Mkutano wa SADC Akimuwakilisha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akielekea kupanda ndege katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako tayari kwa safari ya kurudi Tanzania mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na Waziri wa Elimu ya Juu , Mafunzo na Ubunifu wa Namibia Mhe. Dkt. Itah Kandjii-Murangi  muda mfupi kabla ya kupanda ndege katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako tayari kwa safari ya kurudi Tanzania mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiaga Viongozi waliomsindikiza katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako tayari kwa safari ya kurudi Tanzania mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) . (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.