Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, Azungumza na Makamishana wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar na Uongozi wa Wizara ya Habari na Mambo ya Kale Zanzibar Ikulu leo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza wakati wa Mkutano wake na Makamishna wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar na Uongozi wa Wizara ya Habari na Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, na Kamisheni ya Utalii, uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu leo. kuzungumzia Sekta ya Utalii. akionesha picha ya majengo itakayokuwa katika eneo la Bungi kwa Bihole Wilaya ya Kati Unguja Mkoa wa Kusini Unguja.
Makamishna wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar wakifuatilia mkutano huo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumzia Sekta ya Utalii Zanzibar, mkutano huo umewakutanisha Uongozi wa Kamisheni ya Utalii na Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Said Hassan Said, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar Ndg. Khamis Mussa, Mwenyekiti wa Kamishenin ya Utalii Zanzibar Bi. Sabaah Saleh, wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza wakati wa mkutano huo uliofanyika leo Ikulu Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na Uongozi wa Wizara ya Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar na Uongozi wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar leo. 
Viongozi wa Serikali na wa Wizara ya Habari Utalii na Mambo ya Kale na Makamishna wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar wakiwa katika ukumbi wa mkutano Ikulu Zanzibar wakifuatilia mkutano huo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, kuzungumzia Sekta ya Utalii Zanzibar.
Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar Dkt. Abdallah Mohammed Juma, akizungumza wakati wa mkutano huo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, uliofanyika ukumbi wa Ikulu Leo.
Mkurugenzi Masoko waKamisheni ya Utalii Zanzibar Dkt. Miraj, akizungumza wakati wa mkutano huo uliofanyika Ikulu leo, kuhusiana na Sekta ya Utalii Zanzibar. 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, akizungumza wakati wa mkutano huo na Uongozi wa Wizara ya Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar pamoja na Makamishna wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, kushoto Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein na kulia Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mhe.Mahmoud Thabit Kombo.






No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.