Balozi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu (UAE) Mhe.Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, kulia akiwasikilisha Salamu za rambirambi kwa Niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt. Ali Mohamed Shein kwa Mtawala wa Sharjah Sheikh Khalid bin Sultan Mohammed Al Qasimi,hafla hiyo imefanyika katika makazi yake Sharjah.
MTAWALA wa
Sharjah Sheikh Sultan Bin Mohammad Al Qasimi
amepokea salamu za rambirambi kutoka kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein alizozituma kwa Mtawala huyo wa
Sharjah kufuatia kifo cha mwanawe Sheikh Khalid bin Sultan bin Mohammad Al
Qasimi.
Akipokea salamu hizo za rambirambi
zilizowasilishwa na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa
Nchi za Falme za Kiarabu (UAE) Balozi
Mbarouk Nassor Mbarouk, Sheikh Sultan Bin Mohammad Al Qasimi alitoa
shukurani zake kwa Rais Dk. Shein pamoja na wananchi wote wa Zanzibar kwa kumpa
pole kufuatia msiba huo wa mwanawe.
Kwa mujibu wa maelezo ya Balozi Mbarouk
akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu akiwa ofisini kwake mjini
Abudhabi alisema kuwa Kiongozi huyo wa Sharjah ameleza kufarajika na salamu
hizo za rambirambi alizozituma Dk. Shein huku akisifu na kupongeza uhusiano na
ushirikiano wa kihistoria uliopo kati ya Sharja na Zanzibar na kuahidi kuuendeleza.
Rais Dk. Shein, alimtumia salamu za
rambirambi Sheikh Sultan Bin Mohammad Al
Qasimi kufuatia kifo cha mwanawe Sheikh Khalid bin Sultan bin Mohammad Al
Qasimi kilichotokea London, nchini
Uingereza Julai 1, mwaka huu.
Katika salamu hizo, Dk.
Shein alieleza kuwa amepokea kwa huzuni kubwa taarifa ya kifo cha mtoto wa
kiongozi huyo na kwa niaba yake binafsi pamoja na wananchi wote wa Zanzibar,
wanatoa salamu zao za pole kwa familia, ndugu na wananchi wote wa Sharjah na
Taifa zima za Umoja wa Falme nchi za Kiarabu kwa jumla.
Salamu hizo zilimuomba
Mwenyezi Mungu awape moyo wa subira familia ya Sheikh Al Qasimi wakiwemo ndugu,
jamaa na marafiki wa Marehemu Sheikh Khalid bin Sultan bin Mohammad Al Qasimi
katika kipindi hiki kigumu cha msiba huku akimuomba Mwenyezi Mungu kumlaza
mahala pema peponi, Amin.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment