Habari za Punde

Uzinduzi wa Kongamano la Namthamini Mwanamke Wilaya ya Magharibi

 Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi akivishwa Skafu mara baada ya kuwasili Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Magharibi “A”  kufungua Kongamano la Siku mbili la Namthamini Mwanamke.
 Mama Asha Suleiman Iddi kufungua Kongamano la Siku mbili la Namthamini Mwanamke lililoandaliwa na Uongozi wa Kamati ya Afya na Mazingira ya UVCCM Mkoa Magharibi hapo Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magharibi.

 Baadhi ya Washiriki wa Kongamano la Siku mbili la Namthamini Mwanamke wakimsikiliza Mama Asha hayupo pichani wakati akilifungua Kongamano hilo.





 Mshauri wa Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mzee Abdullah Mwinyi akitoa neno la shukrani mara baada ya uzinduzi wa Kongamano la Namthamini Mwanamke.
 Mama Asha Suleiman Iddi akipokea zawadi Maalum kutoka kwa Uongozi wa Kampuni ya Yammy Yami inayosambaza Bidhaa za Pempas hapa Nchini ambayo ndio iliyodhamini Kongamano la Vijana.
Mwenyekiti wa Chipukizi Mkoa Magharibi Kijana Rukaya Maktuba  akitoa salamu za Chipukizi kwa kuitaka Jamii kupiga mstari mwekundu katika kukomesha vitendo vya udhalilishaji Nchini.
Picha na – OMPR – ZNZ.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.