Na Miza Othman – Maelezo Pemba.
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba.Mhe. Omar Khamis Othman ametaka wamiliki wa Hoteli kufuata Sheria na Utaratibu uliowekwa ili kuepusha migogoro isiyokuwa ya lazima baina yao na Serikali.
Aliyasema hayo wakati akipokuwa akizungumza na Wajumbe kutoka Taasisi mbalimbali juu ya uwajibikaji na kuheshimu muongozo wa utekelezaji wa majukumu yao huko katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa .
Hata hivyo amewataka wajumbe hao kutofanya kazi kwa mazowea ili kuepusha muhali kwa wamiliki wa Hotel hizo kwani kufanya hivyo kutapelekea kuzotesha maendeleo ya Serikali katika Nchi yao.
“Watu wote ni watalii ikiwa Mweupe au mweusi tusidharau kitu twende kwa pamoja ili Zanzibar iwesalama”, alisema Mkuu wa Mkoa Omar Kahamis.
Aidha wamiliki wa Hoteli wametakiwa kuheshimu watu wote kwani kufanya hivyo ni kuzipahadhi Hoteli zao na pata wateja kwa urahisi ili kuingiza kipato kwa haraka na kuweza kuondoa changamoto zinazo wakbili katika kazi zao.
Nae Mukurugenzi kutoka Idara ya Uwezeshaji na Maendeleo ya Mradi (ZIPA) Shariff Ali Shariff amesema lengo na madhumuni ni kuwakumbusha wamiliki wa Hoteli kuzifuwata sheria za kazi katika Utekelezaji wa majukumu yao ili kuondokana na chanagamoto zisizokuwa za lazima baina ya Hoteli na Serikali.
Pia Mkurugenzi huyo amesema Serikali ipo katika kutekeleza na kusimamia majukumu yake bali si kuwaonea wamiliki wa hoteli hizo.
“Nilazima Wajumbe wote wafuwate utaratibu na muongozo uliyoekwa ili kukamilisha lengo walilokusudia katika utekelezaji wa kazi yao”, Alisema Mkurugenzi Shariffu Ali.
Wajumbe walioshiriki katika Mkutano huo wamesema nilazima watumie gharama na kuchagua watu madhubuti ili kuweza kupata taarifa za kila siku sio kutegemea wamiliki wa Hoteli kwani wanaweza kuwatumia taarifa zisizo za uhakika.
Hata hivyo wajumbe hao wamesema ni lazima wapewe nguvu na Viongozi wao ili kuweza kufanya kazi kwa uzalendo na sio kwa mazoea kwani kufanya hivyo kutapelekea kukamilisha kwa urahisi.
“ Watu wawe siriasi katika kutekelea majukumu yao na sio kuoneana umhali’, walisema wajumbe hao.
Jumla ya Hoteli 9n zitatembelewa na wajumbe ulioandaliwa na Serikali ili kujua sharia zinazofuatwa katika Hoteli hizo.
No comments:
Post a Comment