Habari za Punde

ZEC yaendelea kugawa vitambulisho vya kupigia kura Wilaya za Unguja



Na Jaala Makame Haji --- ZEC

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC imeendelea na kazi ya ugawaji wa vitambulisho vya kupigia katika vituo 272 vilivyotumika katika kazi ya Uandikishaji wa Wapiga Kura Wapya na uhakiki wa taarifa za Wapiga Kura kwa maeneo mbali mbali ya Unguja.

Kazi hiyo inafanyika kwa siku mbili katika kila kituo baada kwa Wilaya zote za Unguja ambapo awali ilifanyika katika vituo 135 vya Wilaya ya Pemba tarehe 18 hadi 19 mwezi huu.

Wakizungumza baadhi ya Wapiga Kura waliofika vituoni kwa lengo la kuchukua vitambulisho vyao vya kupigia kura walisema kazi inaendelea vizuri kutokana na utaratibu mzuri wa ulioandaliwa na Tume katika ugawaji wa vitambulisho hivyo.

Walisema kuwa, utayari wa wapiga kura kufika vituoni kuchukua vitambulisho vyao unatokana na juhudi zinazochukuliwa na Tume pamoja na upatikanaji wa taarifa sahihi kupitia vyombo vya habari.

Walifafanua kuwa, ZEC kabla ya kazi hii, ilitoa elimu ya Wapiga Kura kupitia redio, TV na mitandao ya kijamii ambapo walisambaza namba za kupiga kupitia mtandao wa Zantel ambazo ziliwasaidia Wapiga Kura kujua vituo ambavyo vitambulisho vyao vinapatikana pamoja na kujua namba ya box la kitambulisho.

Mkurugenzi Baraza la Manispaa Wilaya ya Magharib “A” AMOUR ALI MUSSA ambaye ni miongoni mwa Wapiga Kura waliofika vituoni kuchukua kitambulisho hich ameeleza kuridhika kwake na mwenendo na utaratibu wa ugawaji wa vitambulisho ambapo ametoa wito kwa Wananchi kujitokeza kwa wingi kuchukukua vitambulisho ambavyo vitawawezesha kupiga kura na kuchakua viongozi wanaowataka.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.