Habari za Punde

MAJALIWA ATEMBELEA MAONESHO YA NANE NANE UWANJA WA NYAKABINDI SIMIYU

Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akikagua bustani ya kabeji wakati alipotembelea banda la Jeshi la Magereza katika Kilele cha Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Wakulima Nane Nane kwenye uwanja wa Nyakabindi mkoani Simiyu,
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu kifaa kinachotumika kutambua aina ya dawa za kulevya alizotumia mtu kutoka kwa Mfamasia wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Samwel Mbesere (kulia) wakati alipotembelea banda la mamlaka hiyo  katika Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Wakulima Nane Nane kwenye uwanja wa Nyakabindi mkoani Simiyu, Agosti 8, 2020. Wa pili kushoto ni Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na  Dawa za Kulevya, James Kaji.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akishuhudia wakati George Eliasi  alipokuwa akisafisha mkonge  kwa kutumia mashine iliyotengezwa Kishapu na mbunifu  Daudi Magili (hayupo pichani) wakati alipotembelea Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Wakulima Nane Nane kwenye uwanja wa Nyakabindi mkoani Simiyu, Agosti 8, 2020. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Bibi Zainab Telack.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama mashine ya kubana singa za mkonge (Pressing Mashine)  wakati alipotembelea Maonesho  ya Kilimo na Sherehe za Wakulima Nane Nane kwenye uwanja wa Nyakabindi mkoani Simiyu, Agosti 8, 2020. Mashine hiyo imetengenezwa Kishapu na mbunifu  Daudi Magili. 


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.