Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi amezindua mtambo wa kuzima moto wenye gharama ya milioni 779.3 ulionunuliwa kutoka kikosi cha Nyumbu/SUMA JKT kwa ajili ya kuzimia moto katika shamba la miti la Sao hill ambo limekuwa likibeba uchumi wa wilaya ya Mufindi
Huo ndio mtambo wenyewe wa kuzimia moto katika shamba la Sao Hill aliouzindua Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi
Huo ndio mtambo wenyewe wa kuzimia moto katika shamba la Sao Hill aliouzindua Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi
Huo ndio mtambo wenyewe wa kuzimia moto katika shamba la Sao Hill aliouzindua Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi ukiwa unauwezo wa kurusha maji zaidi ya mita mia moja.
NA FREDY
MGUNDA,IRINGA.
Mkuu wa
mkoa wa Iringa Ally Hapi amezindua mtambo wa kuzima moto wenye gharama ya
milioni 779.3 ulionunuliwa kutoka kikosi cha Nyumbu/SUMA JKT kwa ajili ya
kuzimia moto katika shamba la miti la Sao hill ambo limekuwa likibeba uchumi wa
wilaya ya Mufindi
Akizungumza
kabla ya uzinduzi wa mtambo huu Mhifadhi mkuu wa shamba la miti Sao hill Juma
Mwita alisema kuwa lengo la kununua mtambo huu ilikuwa ni kuhakikisha
wanaendelea kupambana na majanga ya moto ambayo yamekuwa yanatokea mara kwa
mara na kuleta athari kwa serikali.
Mwita alisema
kuwa shamba la miti la Sao Hill lina umuhimu mkubwa kiuchumi,kijamii na
kimazingira kwa taifa la Tanzania na duniani kwa ujumla kutokana na namna
shamba lilivyo hifadhiwa.
“Shamba hili
ni kichecheo kikubwa cha ujenzi wa uchumi wa viwanda kutokana na kuwa chanzo
cha malighafi ya viwanda vikubwa,vya kati na vidogo ambavyo hutengeneza bidhaa
mbalimbali zinazotokana na mazao ya misitu” alisema
Aliongeza kuwa
kuwa TFS kwa kushirikiana na wadau wengine na uongozi wa wilaya utaendelea
kujipanga kikamilifu ili kuhakikisha majanga ya moto yanadhibitiwa katika
shamba la miti la Sao Hill.
Mwita alisema
kuwa wamekuwa wakitoa elimu na vifaa vya kuzimia moto kwa wananchi
wanaolizunguka shamba hilo mara kwa mara kwa lengo la kuendelea kuwakumbusha
madhara yanayotokana na moto katika shamba hilo.
Akizungumza
mara baada ya kuzindua mtambo huo wa kuzimia moto Mkuu wa mkoa huyo aliwapoongeza
TFS kwa mchango wao kiasi bilioni tano kama sehehemu ya mchango wao kwa jamiii
kwa kipindi cha awamu ya utawala wa serikali ya awamu ya tano
Licha ya
kuwapongeza Hapi aliwataka wafanyazi wa shamba hilo kuwajibika na kutimiza
wajibu kwenye majukumu ambayo wamepangiwa kuyatumikia kwa lengo la kuleta
maendeleo ya taifa na kukuza uchumi wa wananchi kwa ujumla
Hapi aliwataka viongozi wa TFS waliopo katika shamba la miti la Sao Hill
kuhakikisha wanautunza vilivyo mtambo huo wa kuzimia moto kwa kuwa umekuwa
wakisasa zaidi na unauwezo wa kusaidia kuzima moto katika maeneo mbalimbali ya
wilaya hata mkoa pale inapohitajika.
Aliwaomba wananchi kuacha mara moja tabia ya kuchoma moto kwenye
mashamba ya miti kwa kuwa kufanya hivyo kunarudisha nyuma maendeleo kwa
kufifisha juhudi za kukuza uchumi wa taifa.
No comments:
Post a Comment