Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu
Bi Ruth Minja akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali leo Jijini Dodoma
kuhusu mfumuko wa bei kwa mwezi wa Agosti, 2020 ambapo Tanzania ni asilimia 3.3 na inaendelea kufanya vizuri ikilinganishwa na nchi za Kenya kwa asilimia
4.36 na Uganda asilimia4.7
Na
Mwandishi wetu- Dodoma
Tanzania yaendelea
kufanya vizuri Mfumuko wa Bei wa Taifa
kwa mwaka ulioshia mwezi Julai, 2020 ambao ni asilimia 3.3 kutoka asilimia 3.2
kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2020 ikilinganishwa na Kenya asilimia 4.36 na
Uganda asilimia 4.7
Akizungumza leo,
Jijini Dodoma Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii Bi Ruth Minja amesema
kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi
Julai, 2020 umeongezeka kidogo ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka
ulioishia mwezi Juni, 2020.
Akifafanua amesema
kuwa baadhi ya bidhaa za vyakula zilizoongezeka kwa mwezi Julai ni pamoja na;
unga wa mahindi kwa asilimia 7.9, mtama asilimia 4.8, unga wa muhogo kwa
asilimia 3.0, dagaa asilimia 3.8, matunda asilimia 4.0, mbogamboga asilimia
9.6.
Aliongeza kuwa,
Baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizoongezeka bei kwa mwezi Julai, 2020
zikilinganishwa na zile za Julai, 2019 ni pamoja na; mavazi kwa asilimia 2.8,
gesi ya kupikia kwa asilimia 5.9, samani kwa asilimia 2.7, gharama za
utengenezaji na ukarabati wa nyumba kwa asilimia 6.2 na mkaa kwa asilimia 11.6.
“Nchini Kenya Mfumuko
wa Bei kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2020 ni asilimia 4.36 kutoka asilimia
4.59 kwa mwaka unaoishia mwezi Juni 2020, kwa upande wa Uganda, Mfumuko wa Bei
kwa mwaka ulioishia Julai, 2020 umeongezeka hadi asilimia 4.7 kutoka 4.1 kwa
mwaka ulioishia mwezi Juni, 2020”, Alisisitiza Bi Minja
Ofisi ya Taifa ya
Takwimu (NBS) imepewa mamlaka ya kutoa, kusimamia na kuratibu upatikanaji na
usambazaji wa Takwimu Rasmi nchini ikiwa ni pamoja na takwimu za Mfumuko wa Bei
kwa ajili ya matumizi ya Serikali na wadau wa takwimu.
No comments:
Post a Comment