Mwakilishi wa Kikundi cha
Wanawake wanaofanya Sanaa ya Uchoraji Safina Kipokota (kushoto) akimkabidhi
zawadi Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji
Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi,leo Desemba 04,2020, Jijini Dar es Salaam,
katika kikao na wadau wa Sanaa za Ufundi
kujadili namna ya kuendeleza tasnia ya hiyo kufuatia tamko la Mhe.Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kuendeleza Sanaa
alipokuwa akifungua bunge.
Na.Anitha Jonas – WHUSM, Dar es Salaam. 05/12/2020
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na
Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbasi amesema kuanzia mwaka 2021 kutakuwa
Maonesho ya Kitaifa ya Sanaa za Ufundi nchini.
Dkt. Abbasi ametoa kauli hiyo leo Desemba 03, Jijini Dar
es Salaam, katika mkutano na Wasanii wa Sanaa za Ufundi ikiwa ni mwendelezo wa
vikao vyake vya kukutana na makundi mbalimbali ya wadau wa Sanaa kwa lengo la
kujadili namna ya kukuza na kuendeleza sekta ya Sanaa kwa kuzingatia ahadi ya
Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli katika
hotuba yake wakati akifungua Bunge.
Akizungumza katika kikao
hicho Dkt.Abbasi alisisitiza kuwa serikali imedhamiria kusaidia sekta ya
sanaa, kwa kukuza masoko na kujenga mazingira rafiki ya kuendeleza sanaa
nchini.
"Viongozi wa Mashirikisho na vyama nendeni mkafanye utafiti
wa Maonesho ya kazi za Sanaa za Ufundi Kimataifa na mnilete kalenda
inayoonyesha matukio hayo, na nchi inayoandaa maonesho hayo ili
tuwasiliane na balozi zetu kuona namna tunaweza kuwasaidia, sisi pia kama
wizara kila patakapo kuwa na matukio makubwa au mechi kubwa pale Uwanja wa
Benjamin Mkapa nitatoa eneo kwa wasanii wa Sanaa za Ufundi kuonyesha na
kuuza kazi zao,"alisema Dkt.Abbasi.
Akizungumza katika kikao hicho Dkt.Abbasi alisisitiza
wasanii kutumia vyama vyao na Mashirikisho kutoa maoni ya mambo wanayokwamisha uendeshaji
wa kazi zao ikiwemo utitiri wa kodi na tozo ambazo nikubwa zinazokwamisha
shughuli hizo.
Naye Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa Taifa Godfrey Mngereza
ahidi kupokea maoni yote ya wadau hao na kusema atayafanyia kazi ikiwemo
kuandaa mpango wa kutoa mafunzo kwa wasanii wa Sanaa za Ufundi ya namna ya
kufanya biashara katika mfumo wa kisasa kwa kuweka kipao mbele thamani ya kazi
zao.
Halikadhalika nae Msanii wa Sanaa ya Uchoraji Hasmain Raza
alitoa ombi kwa Serikali la kuangalia muundo wa majukumu kwa taasisi ya BASATA
katika uendeshaji, kwa kuomba ianzishe Idara au Vitengo cha Muziki kwa kila
sanaa wanayoisimamia, badala ya sasa hali ilivyo sasa vitu vyote kuendeshwa kwa
pamoja.
No comments:
Post a Comment