Habari za Punde

Profesa Mbarawa atimiza ahadi kwa wakulima bonde la Darajani , Makombeni kisiwani Pemba

KATIBU wa Mbunge wa Jimbo la Mkoani Mariam Said Khamis (kulia) akimkabidhi mita 50 za mpira wa maji, Mwenyekiti wa bonde la Darajani Makombeni Nassor Hakim Haji, uliotolewa na Mbunge wa jimbo hilo Profesa Makame Mbarawa Mnyaa ikiwa ni ahadi yake kwa wakulima hao.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

KATIBU wa Mbunge wa Jimbo la Mkoani Mariam Said Khamis (kulia) akimkabidhi mita 50 za mpira wa maji, Mwenyekiti wa bonde la Darajani Makombeni Nassor Hakim Haji, uliotolewa na Mbunge wa jimbo hilo Profesa Makame Mbarawa mnyaa ikiwa ni ahadi yake kwa wakulima hao.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MAFUNDI kutoka Mamlaka ya Maji Zanzibar ofisi ya Pemba (ZAWA), wakiteremsha mchikichi(mashine ya maji)ndani ya kisima pamoja na mpira wake wa kutolea maji, kwa ajili ya umwagiliaji wa bonde la Kindani Darajani Makombeni, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya mbunge wa jimbo la Mkoani.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

WANANCHI wakinawa mikono baada ya kumalizika kazi ya usafishaji wa kisima cha maji pamoja na uwekaji wa mpira mpya mita 50 ndani ya kisima hicho, ili wakulima wa mpunga bonde la Kindani Darajani makombeni waweze kutumia katika umwagiliaji.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

BAADHI ya mashamba ya mpunga ya umwagiliaji maji katika bonde la Kindani Darajani Makombeni, wakisubiri maji baada ya kulitaayarisha shamba kwa ajili ya kilimo cha awamu ya pili cha mpunga.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.