STATE HOUSE
ZANZIBAR
OFFICE
OF THE PRESS SECRETARY
PRESS
RELEASE
Zanzibar January 10, 2021
RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewataka
wanafunzi kutumia vyema fursa za kuwepo miundombinu bora ya masomo kwa kusoma kwa bidii na nidhamu.
Dk.
Mwinyi amesema hayo leo katika Ufunguzi wa Skuli ya Sekondari ya Hasnuu Makame
, iliopo Kibuteni Mkoa Kusini Unguja.
Amesema
wanafunzi watakaopata nafasi ya kusoma katika skuli hiyo wanapaswa kutumia
vyema fursa hiyo kwa kusoma kwa bidii, ili waweze kufaulu katika amsomo yao
badala ya kujihusisha na masuala yatakayosababisha
kuharibikiwa katika maisha yao ya baadae.
Alisema
ni matumaini yake kuwa wanafunzi watakaosoma skuli hiyo watafulu vyema katika
mitihani yao ya Taifa, kw akuwa skuli
hiyo iko katika mazingira mazuri, walimu wazuri pamoja na kuwa na vifaa vya
kutosha.
Aidha,
aliwataka wakuu wa Wilaya na mikoa kushirikiana na wananchi ili kufanikisha
wanafunzi wote watakaotoka katika skuli 34 za Sekondari mkoani humona kujiunga
katika Skuli hiyo wanafaulu vizuri.
Vile
vile aliwataka walimu kutekeleza ipasavyo wajibu wao wa kusomesha vizuri pamoja
na wazazi na walezi kufuatilia maendeleo ya elimu ya watoto wao ili kubaini
chanagmoto zinazoweza kujitokeza.
Kuhusina
na ujenzi wa majengo hayo, Dk. Mwinyi alisema anaridhishwa na ubora wa majengo
yaliopo katika skuli hapo, na akasisitiza kuwa kuanzia sasa Serikali
haitovumilia kuona inakuwepo miradi inayojengwa chini ya kiwango.
“Miradi
itakayojengwa chini ya kiwango sasa basi, lazima matumizi ya fedha yaendane na
thamani hali ya majengo, tutamchukulia hatua kiongozi yoyote atakejinufaisha
kupitia miradi ya Serikali”, alisema.
Aliahidi
kushirikiana na Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Kiuchumi (BADEA) pamoja na kumpongeza
Mkandarasi wa ujenzi huo Kampuni ya RUINS
kwa kazi kubwa na nzuri ya kukamilisha ujenzi wa majengo hayo.
Aidha,
aliipongeza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa kusimamia vyema miradi ya
elimu, sambamba na kuitaka kujenga viwanja katika eneo la skuli hiyo ili
wanafunzi wapate fursa ya kucheza pamoja na kuagiza eneo la skuli hiyo kupimwa
ili kuzuia uvamizi wa ardhi.
Katika
hatua nyengine, Dk. Mwinyi alipongeza juhudi kubwa zilizofanya na Serikali za
Awamu ziliotangulia, akibainisha kazi kubwa imefanyika kuinua kiwango cha elimu
nchini.
Alitoa
pongezi maalum kwa Uongozi wa Serikali ya Awamu ya saba chini ya Dk. Ali
Mohamed Shein kwa juhudi kubwa za kuinua sekta ya elimu nchini, ikiwemo ujenzi
wa majengo ya ghorofa, ununuzi wa madawati, kuongeza idadi ya walimu, kuondoa
michango kwa wanafunzi, kuongeza bajeti ya mikopo ya elimu ya juu pamoja na
kukiimarisha Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA).
Alisema
kwa kutambua umuhimu kwa maendeleo nchini, Serikali itaendelea na juhudi za
kuyafanyia matengenzo majengo ya skuli pamoja na kujenga mapya, kuongeza
upatikanaji wa vifaa, kupitia upya mitaala ya elimu pamoja na kuzingatia
maslahi ya walimu, ikiwa ni hatua ya utekelzaji wa Ilani ya CCM.
Aidha,
Dk. Mwinyi aliridhia Skuli hiyo kuitwa jina la ‘Hasnuu Makame Secondary school’
kama ilivyopendekezwa.
Mapema, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali
Simai Mohamed Said alitumia fursa hiyo kuwakumbusha wazazi kuzingatia umuhimu wa
kushiriki kikamilifu katika maendleeo ya elimu ya watoto wao.
Nae,
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Mhandisi Dk. Idrissa Muslim
Hija alisema ujenzi wa skuli hiyo
umefanyika kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Benki
ya Kiarabu ya Maendeleo ya Kiuchumi (BADEA) na kugharimu Dola za Kimarekani
Milioni 6.6.
Alisema ujenzi huo unahusisha Majengo mbali mbali,
ikiwemo jengo la Utawala, Dakhalia, nyumba za walimu pamoja na madarasa.
Alieleza
kuwa jengo la Dakhalia lina jumla ya vyumba 38 likiwa na uwezo wa kukaliwa na
wafunzi 152, wakati ambapo kuna madarasa 16 yenye uwezo wa kutumia na wanafunzi
640, ikiwa ni wastani wa wanafunzi 40 kwa darasa moja,
Alisema
miongoni mwa chanagmoto zinazoikabili Skuli hiyo, ni pamoja na ukosefu wa uzio
pamoja na Kampuni ya RUINS kuidai Wizara Elimu na Mafunzo ya Amali kiasi cha
shilingi Milioni 541.7 ikiwa sehemu ya malipo ya Ujenzi wa jingo la Dakhalia ya
wanaume.
Dk.
Idrissa aliwataka wananchi wote wanaozunguka eneo hilo kushirikiana katika kulinda
rasilimali za skuli hiyo kwa faida ya vizazi vijavyo.
Katika
hafla hiyo Viongozi mbali mbali wa Kitaifa walihudhuria, akiwemo Makamo wa Pili
wa Rais Hemed Suleiman Abdulla, Makamo wa Pili wa Rais mstaafu Balozi Seif Ali
Idd, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na
Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said, Katibu Mkuu wa CCM Abdalla Juma
Sadalla, Mawaziri pamoja na wananchi wa shehiya mbali mbali za Mkoa Kusini Unguja.
Abdi
Shamna, Ikulu Zanzibar
No comments:
Post a Comment