Dkt. Peter Mataba akiwasilisha mada kuhusu Mkakati wa Mawasiliano katika taasisi
za Umma.
Innocent Mungy akiwasilisha mada kuhusu “uandaaji wa
Mkakati wa Mawasiliano na utekelezaji wake”
Katibu Mkuu wa Habari Dkt. Hassan Abbasi (katikati) na Naibu wake Dkt. Ally Possi (kulia) wakiongoza Kikao cha 16 cha Maafisa Habari Jijini Mbeya. Kushoto ni Aidan Eyakuze Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza.
Na John Mapepele, Mbeya
Katibu Mkuu wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi amewataka Maafisa Habari,Mawasiliano
na Uhusiano kote nchini kuzingatia maelekezo, mbalimbali ya viongozi wakuu
na miongozo inayotolewa na Serikali
wakati wanapoandaa mikakati ya
mawasiliano kwenye maeneo yao
Dkt Abbasi ambaye ni mtaalam
mbobezi kwenye taaluma ya Habari ametoa kauli hiyo Mei 25, 2021 wakati akichangia
uzoefu wake kwenye mada ya” uandaaji wa Mkakati wa Mawasiliano
na utekelezaji wake” iliyowasilishwa na mwanahabari mkongwe, Innocent Mungy
kwenye kikao kazi cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano (TAGCO) kinachoendelea
Jijini Mbeya.
Amesema Serikali imekuwa na maelekezo
mahususi ya kimkakati ambayo ni muhimu kuyaingiza ili kuleta matokeo bora
wakati wa kufanya tathmini ya utendaji wa kazi za taasisi za Serikali.
Akiwasilisha mada hiyo Mungy
amesisitiza kuwa wakati wa sasa mkakati wa mawasiliano ni nyenzo muhimu
inayosaidia taasisi kufanya kazi kwenye kiwango kinachopimika.
Mwenyekiti wa kikao kazi
hicho ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Ally Possi alitaka
ufafanuzi wa namna gani Maafisa Habari wanaweza wakawafanya baadhi ya viongozi wasiopenda
na kutambua umuhimu wa kuwa na mikakati
ya mawasiliano kwenye maeneo yao ambapo ilielezwa kuwa ni kwa kuwashirikisha.
Naye Dkt Peter Mataba wakati
akiwasilisha mada ya “Mkakati wa Mawasiliano” amesisitiza kuwa taasisi zinapaswa
kuzingatia ujumbe unaopelekwa kwa hadhira, na malengo ya taasisi husika ambayo
yanatekelezeka kulingana na Mpango Mkakati wa taasisi husika.
No comments:
Post a Comment