Habari za Punde

Mahafali ya Saba ya Chuo cha Tabora Polytechinic. Elimu Ndio Ufunguo Nuru na Mwanga wa Maisha.

mkuu wa wilaya ya Tabora mjini na ambaye Mgeni Rasmi Dkt Yahya Nawanda akiongea na wananchuo wa Tabora Polytechnic College jana .
Mkurugenzi wa Chuo Cha Tabora Polytechnic College Bw.Shabani Mrutu akizungumza wakati wa mahafali ya Saba ya Chuo hicho yaliofanyika katika viwanja vya Chuo Mkoani Tabora.
Wahitimu wa Chuo cha Tabora Polytechinic wakishiriki katika hafla ya Mahafali ya Saba ya Chuo hicho yaliofanyika katika viwanja vya Chuo Mkoani Tabora.
Mkuu wa Wilaya ya Tabora Dkt.Yahya Nawanda akiwa katika picha ya pamoja na Wahitimu wa Mahafali ya Saba ya Chuo cha Tabora Polytechinic, yaliofanyika katika viwanja vya Chuo hicho Mkoani Tabora.

Na Lucas Raphael,Tabora

Mkuu wa wilaya Tabora  Dkt Yahya Nawanda amewataka wazazi na walezi mkoani hapa kuwekeza kwenye elimu ya watoto wao kwani elimu ndio Nuru na mwanaga wa maisha yao ya baadaye.

Alitoa wito huo katika mahafali ya saba ya chuo cha Tabora Polytechinic College yaliyofanyka kwenye kiwanja cha chuo hicho kilichopo  kata ya Mpera manispaa ya Tabora jana.

Alisema kwamba wazazi na walezi wanajukumu kubwa la kuhakikisha watoto wao wanapata elimu nzuri na bora kwani maisha bila elimu ni sawa na kukosa mwanga kwenye maisha ya utandawazi.

Aidha aliwapongeza wazazi na walezi wanaosomesha watoto wao kwa kunyima kwa kulipa ada kila baada ya muhula wa masomo kwani kufanya hivyo unamwekea mazingira na mwanga bora na nuru njema mtoto ili kuweza kufanikiwa kwenye maisha ya baadaye .

Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya aliwataka wazazi na walezi kuhakikisha wanawalinda watoto wao na kuwawekekea  mazingira bora ya maisha   kwa kuepukana na vishawishi vinavyoweza kusababisha kujiingiza kwenye vitendo vya kihalifu .

 

Alisema kwamba katu hatoweza kuona vitendo hivyo vikifanyika wilani humo badala yake wahalifu wote watakutana na mkono wa  sheria .

Awali Mkurugenzi wa Chuo Cha Tabora Polytechnic College Shabani Mrutu alimweleza  mkuu wa wilya hiyo ambaye alikuwa mgeni Rasmi wa mahafali hayo ya saba Dkt Yahya

 Nawanda kuwa chuo hicho kina changamoto  za usalama mdogo katika maeneo ya chuo nyakati za usiku.

 

Aidha alisema kwamba changamoto zingine ni wazazi kuwa na uwezo mdogo wa kulipa ada na kusababisha mwanafunzi kuendelea ma masomo , Lakini chuo hicho kina mipango   mikakati ya chuo ni  kuendelea kuwekeza kwenye wakufunzi wenye sifa,  vifaa vya kufundishia na kujifunzia ili chuo kiendelee kuwa bora na kimbilio la vijana wa Tabora.

 

Mrutu alisema kwamba malengo mengine ni kujenga hospitali ya kisasa , kuendelea kushirikiana na jamii inayowazunguka na kutoa huduma ya afya bure kwa jamii.

 

Alisema chuo kimefanikiwa katika nyanja mbalimbali kutoka kwenye majengo ya kupanga na kujenga majengo ya yenyewe , kusajili chuo, kutoa wahitimu zaidi ya 1,000  na kujiunga na vyuo vikuu ndani na nje ya nchi

 

Alisema chuo hicho kina kozi 10 ambacho kilianzishwa ili kuitikia wito wa serikali kuzitaka sekta binafsi nchini kuwekeza elimu ya ufundi ili kuweza kuandaa wataalam watakaosaidia ukuaji wa uchumi wa sekta ya viwanda.

 

Mkurugenzi Mrutu alisema kwamba chuo hicho kilianzishwa mwaka 2004 kikiwa na jina la Musoma Utalii College, hapo awali kilikuwa na fani 2 ambazo ni Uongozaji wa watalii na Usimamizi wa Hoteli chini ya usajili wa VETA.

 

Aidha  alimueleza mkuu wa wilaya kwamba hapo awali chuo hicho kilianza ma wanafunzi 42 na wakufunzi 4 na kiliendelea kukua hadi 2012 kiliposajiliwa na Baraza la Elimu ya ufundi la Taifa NACTE.

 

Katika mahafali hayo waliohitimu ni wanachuao 290 kutoka katika fani za Ufamasia ,Utabibu , Maabara ,Tehama Waongza watalii ,Watunza Kumbukumbu ,Waandishi wa habari na Utangazaji na Walimu wa Elimu ya Awali.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.