Habari za Punde

Mfumo wa Kielektoroniki wa Uratibu na Ufuatiliaji wa Shughuli za Serikali Wazizinduliwa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akitoa hotuba fupi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mfumo wa Kielektroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za Serikali (DashBoard) iliyofanyika kwenye ukumbi wa Kambarage, Jengo la Hazina.

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) akieleza jambo wakati wa hafla hiyo.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Tixon Nzunda akieleza jambo wakati wa hafla ya kuzindua rasmi Mfumo wa Kielektroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za Serikali (DashBoard) kwenye ukumbi wa Kambarage, Jengo la Hazina
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akitoa hotuba fupi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mfumo wa Kielektroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za Serikali (DashBoard) iliyofanyika kwenye ukumbi wa Kambarage, Jengo la Hazina
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akitoa hotuba fupi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mfumo wa Kielektroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za Serikali (DashBoard) iliyofanyika kwenye ukumbi wa Kambarage, Jengo la Hazina
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (katikati) akizindua rasmi Mfumo wa Kielektroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za Serikali (DashBoard) kwenye ukumbi wa Kambarage, Jengo la Hazina tarehe 16 Agosti, 2021, Jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Mhandisi Hamad Masauni. Kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Tixon Nzunda.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (katikati) akiangalia Mfumo wa Kielektroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za Serikali (DashBoard) mara baada ya kuuzindua rasmi kwenye ukumbi wa Kambarage, Jengo la Hazina tarehe 16 Agosti, 2021, Jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Mhandisi Hamad Masauni. Kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Tixon Nzunda.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Naibu Mawaziri walioshiriki katika hafla ya uzinduzi wa Mfumo wa Kielektroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za Serikali (DashBoard), Jijini Dodoma. Kushoto aliyekaa ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Tixon Nzunda.

Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu.

(SERA, URATIBU, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)

Na: Mwandishi Wetu – Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia maswala ya Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amezindua rasmi mfumo wa kielekroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za serikali ambao utawezesha kuimarisha uratibu wa shughuli za Serikali ikiwemo upatikanaji wa taarifa za utekelezaji kwa wakati.

 

Akizungumza wakati wa tukio la uzinduzi wa Mfumo huo wa Kielektroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za Serikali (DashBoard) hii leo Agosti 16, 2021 alieleza kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu ina jukumu kubwa la kuratibu shughuli zote za Serikali ikiwa ni pamoja na kuratibu usimamizi wa utekelezaji wa Ilani Chama Cha Mapinduzi. Katika uratibu huo, Ofisi hiyo ina wajibu wa kuratibu taarifa kutoka wizara zote na taasisi za Serikali, hivyo kuzijumuisha na kuandaa ripoti ya Serikali ambayo huwasilishwa kwa mwezi, robo mwaka, nusu mwaka na mwaka kulingana na taarifa husika.

 

Waziri Mhagama alibainisha kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu imekuwa ikikabiliana na changamoto ya upatikanaji wa taarifa za utekelezaji na za uhakika kwa wakati, hali hiyo imechangiwa na kutotumia mifumo ya kielektroniki ambayo inarahisisha upatikanaji na uandaaji wa taarifa. Pia, changamoto nyingine ambayo ofisi hiyo au Serikali kwa ujumla inakumbana nayo ni uainishaji wa vigezo vya kupima ufanisi wa utekelezaji katika baadhi ya maeneo hivyo kwa kuzingatia changamoto hizo Ofisi ya Waziri Mkuu iliamua kuboresha Mfumo wa Dashboard ili kuongeza ufanisi na kurahisisha uratibu wa shughuli za Serikali.

 

“Mfumo huu wa Kielektroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za Serikali (DashBoard) utaimarisha uwezo wa Ofisi ya Waziri Mkuu katika kuratibu utekelezaji wa shughuli za Serikali pamoja na kuwezesha kupima ufanisi wa utekelezaji. Kwa sasa mfumo utawezesha upimaji wa utekelezaji wa shughuli za Serikali kwa kutumia viashiria vya utendaji,” alieleza Waziri Mhagama

“Kiu ya Serikali yetu ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ni kuona serikali anayoiongoza inafanya kazi kwa pamoja na kujiratibu. Ni matumaini yangu tukiutumia vyema mfumo huu wa DashBoard utatuletea matokeo chanya na tutaifanya serikali yetu kuweza kutekeleza wajibu wake wa kila siku kwa wananchi” alisema Mhagama

 

Aliongeza kuwa pamoja na mfumo huu kurahisisha uratibu na upatikanaji wa taarifa za utekelezaji wa shughuli za Serikali, pia mfumo huo una faida nyingine nyingi ikiwemo; kuwezesha upatikanaji wa taarifa za utekelezaji na kwa wakati; kuwa na sehemu moja ya kupata taarifa na takwimu sahihi kuhusu utendaji wa Serikali; kuwezesha ufanyaji tathmini na upimaji wa utekelezaji wa majukumu ya Serikali kwa kutumia viashiria na malengo tuliyojiwekea; kupunguza gharama na muda wa uandaaji na uwasilishaji wa taarifa; na kupata nyaraka muhimu ambazo ni dira katika kupanga na kutekeleza shughuli za Serikali.

 

                        Sambamba na hayo Waziri Mhagama amezitaka Wizara zenye sera za muda mrefu ambazo hazijafanyiwa tathmini zinafanyiwa tathmini haraka ili kubaini mahitaji ya kisera yaliyopo na kuandaa mikakati ya kuimarisha utekelezaji wa sera husika kabla ya kuwekwa kwenye mfumo huo mpya. Pamoja na hayo amewahimiza Viongozi wa Wizara mbalimbali kutekeleza maagizo na maelekezo ya Viongozi wa Kitaifa na wahakikishe wanatoa taarifa za utekelezaji wa maagizo hayo kwa wakati.

 

Aidha, Waziri Mhagama alitoa rai kwa wizara zote na taasisi za Serikali kuhakikisha wanawasimamia wataalam wanaohusika katika uwekaji wa taarifa kwenye mfumo huo ili waweze kuweka taarifa zote muhimu kama ilivyokusudiwa.

 

 

Kwa upande wake, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) alisema kuwa mabadiliko haya ya kidigitali yanasaidia kuisongeza Serikali karibu kwa wananchi badala ya wananchi kufuata huduma za serikali kwenye maofisi.

“Uwepo wa mfumo huu ni jambo ambapo tunapaswa kujivunia nalo kwa kuwa Miaka mitano iliyopita zaidi ya asilimia 80 ya mifumo tulikuwa tunanunua kutoka nje ya nje na tulikuwa tukilipia gharama kubwa sana lakini hii leo zaidi ya asilimia 70 ya mifumo yetu inatengenezwa na wataalam wetu wazalendo na hatutumii gharama kubwa kama hapo awali,” alisema Ndugulile

 

Naye, Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Mhandisi Hamad Masauni alieleza kuwa kuzinduliwa kwa mfumo huo wa Kielektroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za Serikali (DashBoard) utaongeza ufanisi wa kazi na uwazi.

 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Tixon Nzunda alisema kuwa katika mfumo huo wa Kielektroniki wa uratibu na ufuatiliaji wa shughuli za Serikali (DashBoard) moduli zimeongezwa kutoka mbili (2) za awali hadi moduli tano (5) ikiwa ni pamoja na Taarifa za utekelezaji wa Ilani ya Chama Tawala kutoka kwenye Wizara, Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa; Moduli ya pili ni taarifa zote kuhusu sera zinazotekelezwa nchini, mikakati ya utekelezaji wa sera na taarifa za tathmini za sera; Moduli ya tatu ni Utendaji wa Wizara kwa kujumuisha muhtasari wa bajeti, kazi za kipaumbele na viashiria vya msingi na namna vinavyotekelezwa; Moduli ya nne ni taarifa ya utekelezaji wa maagiza yanayotolewa na Viongozi wa Kitaifa; na Moduli ya mwisho ni taarifa za utekelezaji wa ahadi za Rais kipindi cha Kampeni ya Uchaguzi Mkuu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.