Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dk.Hussein Ali Mwinyi amepokea Taarifa ya Muelekeo wa Ujenzi wa Miradi miwili mikubwa itakayotekelezwa Zanzibar,ambapo kwa upande wake ametoa Shukurani kwa Mifuko mitano ya Hifadhi ya Jamii Tanzania kwa Hatua huyo iliyofikiwa.
Miradi hio
ambayo inayotarajiwa kutekelezwa ni ujenzi wa kituo kikuu cha Mabasi eneo la Kijagwani
pamoja na kituo kikubwa cha Biashara na Mikutano eneo la Fumba.
Rais Dk.Mwinyi amesema hii ni mara ya kwanza kwa
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii iliyokuwepo upande wa Jamhuri ya Muungano kuwekeza
Zanzibar nakueleza kuwa hilo ni jambo muhimu kwa kuimarisha Muungano,kwa
kuimarisha Biashara na Uchumi Mpya unaotarajiwa kujengwa.
Aidha Rais Dk.Mwinyi amesema kuwa katika Nchi
nyingi duniani Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ndio inayoendesha Uchumi wa Nchi
ambapo ameongeza kuwa kwa Zanzibar anataka hali iwe kama hivyo.
Kuhusu suala la Ujenzi wa Kituo cha Mabasi cha
Kijangwani, Rais Dk.Hussein Ali Mwinyi ameuhakikishia Ujumbe huo kuwa kwa
Upande wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar itahakikisha kwa Muda mfupi kadri
itakavyowezekana kuweka sawa yale yote ambayo yanatakiwa kuwekwa sawa.
Alisema tathmini ya madi wa kituo cha daladala
umeshakamilikana pale serikali itakapokamilisha taratibu za kuwakabidhi eneo
hilo basi kazihiyo itaaza utekelezaji mara moja.
Aidha alisema eneo hilo litakapokamilika litakuwana
maduka 131, maeneo ya kuegesha gari 135, mabasi mabasi 70, ATM 10, maduka
yavyakula matatu na huduma nyengine muhimu.
Alifahamisha kuwa mradi huo utahusisha pia ujenziwa
vituo vidogo vya mabasi katika eneo la Mnazimmoja na Malindi kwa ajili
yakuwaleta wananchi maeneo ya mjini.
Alisema mradi huo utakapokamilika utaondosha keroya
gari kuegeshwa barabarani na litakuwa ndoto kwa Zanzibar.
Mwenyekiti huyo alisema mradi mwengine ni mradi
wakituo cha biashara na Mikutano katika eneo la Fumba lakini bado unatakiwakufanyiwa
tatmini zaidi.
“Mradi huu bado tunataka kuufanyia tatmini zaidi
natumemuomba Rais Mwinyi atupe muda kidogo ili kufanya tathmini hii na mradi
huuutakapokamilika utakuwa na faida kubwa kwa Zanzibar kwani kwa sasa hakuna
kituohichi cha kimataifa cha kisasa kwa Tanzania,” alisema.
Walimpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti waBaraza la Mapinduzi Dk.
Hussein Ali Mwinyi kwa kuwapa nafasi ya kushirikikatika miradi mengine ya
kimaendeleo hapa nchini na waliahidi kuiangalia natathmini itakapoonesha kwamba
miradi hiyo kuitekeleza basi hawatasita kufanyahivyo.
“Leo ni siku muhimu kwetu kwa kuona kwambatunakuwa ni sehemu ya mikakati
ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikaliya Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania ya kuhakikisha tunasogeza mbele gurudumu lamaendeleo hususan kuwekeza
katika miradi hii ambayo mifuko yetu mitano itaonainafaa kwa uwekezaji.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), Dk. Huda Ahmed Yussuf, alisema mradi
huo kwa kiasikikubwa utaweza kupunguza changamoto ya msongamano wa magari
barabarani ikiwemoeneo la skuli ya Kiswandui na Michenzani.
Alisema katika kituo hicho kutakuwa na usafirimaalum utakaotumika kwa
ajili ya kuwapeleka wananchi mjini kwa kutumia mabasi yakisasa ambayo yatatumia
umeme na gesi.
Dk. Huda, alisema mradi huo wa kituo cha kisasacha Mabasi Kijangwani
unatarajia kutumia zaidi ya shilingi bilioni 14 hadikukamilika kwake.
Aliwaomba wananchi wa Zanzibar kushirikiana katika kuona mradi huo
unakamilika ili kubadilisha haiba ya Mji wa Zanzibar na kuwekamazingira mazuri
ya usafiri wa umma.
Imetayarishwa na Kitengo cha Habari
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment