
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) akizungumza na menejimenti ya Wizara ya Maliasili na Utalii mara baada ya kuripoti ofisini Mtumba jijini Dodoma baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Kushoto ni aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye kwa sasa ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb).
Waziri wa
Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ameahidi kushirikiana na
watendaji na watumishi wa Wizara yake katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya
Wizara hiyo.
Ameyasema
hayo leo Aprili 2,2022 alipowasili katika ofisi za Wizara ya Maliasili na
Utalii zilizopo Mtumba jijini Dodoma mara baada ya kuapishwa.
“Niwahakikishie
kwamba niko tayari kuchapa kazi pamoja nanyi, imani kubwa ambayo Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ametupa
hatutamuangusha” Mhe. Chana amesisitiza.
Aidha,
ameweka bayana kuwa yuko tayari kufanya kazi kwa saa 24 bila kikwazo
chochote.
"Mimi
kama Waziri wenu milango iko wazi saa 24, hakuna wakati
sitapatikana iwe ni usiku, iwe asubuhi hata iwe sikukuu na ndio maana ya kuwa
mtumishi wa umma.” Amesisitiza.
Naye,
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) ameeleza kuwa Wizara
imepata mtu sahihi wa kuitoa ilipo na kuisogeza mbele na kwamba Mhe. Pindi
Chana yuko na timu ya watendaji mahiri na wachapakazi.
Kwa
upande wake, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb)
amemkaribisha Waziri Pindi Chana na kumpongeza kwa kuteuliwa kushika wadhifa
huo.
“Tunakukaribisha
sana katika Wizara ya Maliasili na Utalii na kukupongeza sana kwa kuteuliwa
kushika wadhifa wa Waziri wa Maliasili na Utalii”amesema Mhe. Masanja
Waziri wa
Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ameanza kazi leo kwa mara ya
kwanza mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.
Samia Suluhu Hassan.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) (kushoto) akisalimiana na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) mara baada ya kuripoti ofisini Mtumba jijini Dodoma baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) (kushoto) akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Juma S. Mkomi (kulia) mara baada ya kuripoti ofisini Mtumba jijini Dodoma baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Francis Michael na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb).
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) akisalimiana na watumishi mara baada ya kuripoti ofisini Mtumba jijini Dodoma baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Kulia ni aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye kwa sasa ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) na kushoto ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb).
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Francis Michael akizungumza wakati wa kikao cha Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) (wa pili kutoka kushoto) na menejimenti ya Wizara hiyo mara baada ya Waziri kuripoti ofisini Mtumba jijini Dodoma baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akimpongeza na kumkaribisha Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) (wa pili kutoka kushoto) mara baada ya kuripoti ofisini Mtumba jijini Dodoma baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Kushoto ni aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye kwa sasa ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Francis Michael (kulia).

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) akikabidhiwa nyaraka mbalimbali kama ishara ya kukabidhiwa ofisi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Francis Michael (kulia) mara baada ya kuripoti ofisini Mtumba jijini Dodoma baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Wanaoshuhudia ni aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye kwa sasa ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) (kushoto) na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb)(wa pili kutoka kulia).
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) akizungumza na menejimenti ya Wizara ya Maliasili na Utalii mara baada ya kuripoti ofisini Mtumba jijini Dodoma baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
No comments:
Post a Comment