Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Mwinyi Amekutana na Kuzungumza na Balozi wa Sweden Nchini Tanzania

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Balozi wa Sweden Nchini Tanzania Mhe. Charlota Ozaki Macias, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameishukuru Serikali ya Sweden kwa jitihada zake za kuiunga mkono Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuisaidia kwenye masuala mbalimbali ya uchumi na Maendeleo.

Dk. Mwinyi alitoa shukurani hizo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, bi. Charlota Ozaki Macias.

Alisema hatua ya Serikali ya Sweden kuisaidia Zanzibar kwenye sekta za Elimu na kilimo cha baharini, ikiwemo kilimo cha mwani na kuwasaidia kinamama kisiwani Pemba kwenye kilimo cha ufugaji Samaki ni kuendeleza jitihada za Serikali ya awamu ya nane katika kutekeleza adhma yake ya kuongeza ajira kwa wananchi wake hasa kuwainua wananwake kiuchumi.

Dk. Mwinyi aliiomba Serikali ya Sweden kupitia balozi wake huyo kuisaidia Zanzibar kwenye Sekta ya Nishati, alisema Zanzibar inadhamira ya kuzalisha umeme wake hivyo, iko tayari kwajili ya mazungumzo na kampuni yoyote kutoka Sweden ili waanze hatua za upembuzi yakinifu na kueleza kwamba Shirika la Umeme Zanzibar, (ZECO) liko tayari kwa hatua hiyo kuanza wakati wowote.

Alisema ni jambo la faraja endapo Zanzibar ikipata kujitegemea kwenye uzalishaji wa nishati ya umeme, Dk. Mwinyi alimueleza balozi huyo, kwamba Zanzibar inapokea megawatt 100 tuu ambao pia inapata msaada kutoka Tanzania Bara.

Kuhusu dhamira yake ya kuimarisha Uchumi wa Buluu Visiwani, Rais Dk. Mwinyi aliishukuru serikali ya Sweden kwa hatua yake yakuendeleza jitihada zao kwenye sekta hiyo pia alimueleza balozi huyo kwamba miradi wanayoiendeleza kwa wakulima wa mwani na wafugaji samaki kisiwani Pemba, ni hatua ya Serikali kuwainua wananchi kwa kuwawezesha kimaendeleo.

Alisema ukulima wa mwani kwa Zanzibar ni shughuli inayofanywa na kina mama wengi hivyo, aliipongeza Serikali ya Sweden kwa kuwawezesha wanawake hao.

Kuhusu sekta ya Elimu rais Dk. Mwinyi alimueleza mgeni wake huyo kwamba, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imefanikisha miradi mingi ya maendeleo kwenye sekta hiyo na kueleza kwamba bado inahitaji kuungwa mkono kwenye sekta hiyo.

Naye, Balozi wa Sweden nchini Tanzania bi. Charlota Ozaki Macias, alimueleza Dk. Mwinyi kwamba Serikali ya Sweden inafanyakazi kwa karibu zaidi na Serikali ya Mapnduzi ya Zanzibar ambayo alieleza wanashikiriana kwenye Masuala mbalimbali ya maendeleo.

Balozi Charlota alisema wameshirikiana na Wizraya ya Elimu na Mafunzo ya Amali walifanikisha mradi mbalimbali ikiwemo mradi wa kuwapa mafunzo ya vitendo na kuwawezesha vijana na wasichana wengi walioacha skuli kwa kuwafungua kitaaluma na vitendo.

Alisema Serikali yake itashirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutatua tatizo la umeme nakueleza kwamba nchi yake inawataalamu wakutosha kwenye masuala ya nishati.

Aidha, alimuahidi Rais Mwinyi kwamba Serikali ya Sweden na Zanzibar wataendeleza ushirikiano uliopo katika kukuza Sekta ya uwekezaji na kumuahidi kwamba wapotayari kwa hatua za upembuzi yakinifu kwenye masuala ya uwekezaji.

Uhusiano wa Diplomasia baina ya Tanzania na Sweden umeanza miaka 50 iliyopita kwa mataifa hayo mawili, kushirikina kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo, jamii na uchumi kupitia shirika lake la Sida, Sweden imeisaidia sana Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kwenye sekta ya elimu hasa kwenye ujenzi wa skuli, kuongeza vyumba vya madara pamoja na rasilima nyengine za elimu.

Tanzania ina ubalozi wake nchini humo kwenye mji mkuu wa nchi hiyo, Stockholm ambapo Balozi, Grace Alfred Olotu ni Balozi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nchi za Nordic, mataifa ya Baltik na Ukraine.

Nchi ya Sweden yenye mji mkuu wake Stockholm, iko kaskazini mwa bara Ulaya katika penensula ya Scandnavia, inapakana na nchi za Norway kwa upande wa Magharibi na Kaskazini, inakaribiana na nchi ya Finland kwa upande wa Mashariki na Kusini Magharibi iko karibu na Denkmark.

IDARA YA MAWASILINO, IKULU ZANZIBAR 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Balozi wa Sweden Nchini Tanzania Mhe. Charlota Ozaki Macias, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza mgeni wake Balozi wa Sweden Nchini Tanzania Mhe. Charlota Ozaki Macias(kulia kwa Rais) akiwa na ujumbe wake walipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini Tanzania Mhe.Charlota Ozaki Macias, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini Tanzania Mhe.Charlota Ozaki Macias, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Sweden Nchini Tanzania Mhe. Charlota Ozaki Macias, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na mneni wake Balozi wa Sweden Nchini Tanzania Mhe. Charlota Ozaki Macias, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 13-2-2023

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.