Habari za Punde

Mkufunzi Malya Aibuka Mfanyakazi Bora kwa Mwaka 2023.

 

NI MKUFUNZI DENIS KAYOMBO

Wajumbe wakiwa katika zoezi la kuhesabu kura kumchagua Mfanyakazi Bora kwa mwaka 2023. 

Na.Adeladius Makwega-MWANZA

Wafanyakazi wa Chuo Cha Maendeleo ya Michezo Malya, mkoani Mwanza Aprili 13, 2023 wamemchagua mkufunzi Denis Kayombo kuwa mfanyakazi bora kwa mwaka huu katika uchaguzi uliwakusanya wafanyakazi wote wa kada mbalimbali kuelekea Siku ya Wafanyakazi Duniani, Mei Mosi , 2023.

Akizungumza mara baada ya kutangazwa mshindi mwalimu Kayombo alisema,

“Ninawashukuru sana, maana niliamka asubuhi sikuwa na ili wale lile kujua kuwa leo nitachaguliwa kuwa mfanyakazi bora. Asanteni sana kwa kuwa mmeona ninatosha na ninafaa. Mimi na wezangu tuliokuwa katika kinyang’anyiiro hiki sote ni bora. Nilipokuwa napiga kura nilijipigia mwenyewe kwa kuwa nilipendekezwa tu, nikiogopa kukosa kura kabisa, angalau nipate kura hata moja, lakini kumbe wengine mmenipigia! Tushirikiane kukipeleka mbele chuo chetu na kuyafanikisha maslahi mapana ya michezo na taifa letu.”

Katika uchaguzi huo mkufunzi Silveli Hema alipata alipata 6.7% ya kura zote, mkufunzi Idd Luswaga alipata 33.3% ya kura zote na huku mkufunzi Denis Kayombo aliyeshinda alipata 60% ya kura zote.

Akizungumza baada ya kutangazwa matokeo hayo mwakilishi wa TUGHE katika Baraza la Wafanyakazi Bi Rita Samweli alisisitiza,

“Tumeshafanya uchaguzi na tumempata yule ambaye tunamuona ni sahihi kupata nafasi hii, ninachoomba tuendelee kushirikiana, tuendelee kufanya kazi ili tuone tunafanyaje kwa mwenzetu aliyeshinda. Tunawapongeza wote watatu mliopigiwa kura, nyinyi ni wafanyakazi wetu bora lakini jina moja ndilo linalotakiwa.”

Kikao hicho cha uchaguzi kilihitimishwa kwa mwakilishi wa wafanyakazi wa Chuo Cha Maendeleo ya Michezo Malya katika Baraza la Wafanyakazi Wizarani mkufunzi mkuu Joachim Maganga kutoa mrejesho wa Kikao cha Baraza la Wafanyakzi la Machi 2023.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.