Habari za Punde

ACT Wazalendo yanguruma Bumbwini Makoba

Baadhi ya wananachama na wafuasi wa cha ACT Wazalendo wakiwasikiliza viongozi wao wa kitaifa akiwemo Mwenyekiti Babu Juma Duni Haji , Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho kwa Upande wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman , walipohutubiwa huko katika Viwanja vya Bumbwini Makoba leo tarehe 6 Agosti 2023 katika Mkutano wa hadhara wa kukamilisha mzunguko wa mwanzo wa mikutano ya aina hiyo. Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais.

Mwenyekiti wa Ngome ya wanawake Taifa wa chama cha ACT – Wazalendo Pavu Abdalla Juma akizungunza katika mkutano wa hadhara huko Bumbwini Makoba leo tarehe 6 Agosti 2023.

Makamu Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo Mhe. Othman Masoud Othman akizungunza katika Mkutano wa hadhara huko katika viwanja  vya Bumbwini Makoba leo tarehe 06, Agosti, 2023 akiwa katika hatua ya kukamilisha mzunguko wa kwanza wa mikutano ya hadhara ya chama hicho. ( Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais.

Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa Babu Juma Duni Haji akizungunza na wanachama na wafuasi wa chama hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika huko Bumbwini Makoba Makoba Kaskazini B Unguja leo tarehe 06, Agosti 2023.

 

MWENYEKITI wa Chama cha ACT -Wazalendo Taifa ndugu Juma Duni Haji, amesema kwamba ni muhimu wazanzibari kushirikamana kuwa wamoja ili kutengeneza hatma njema ya kizazi cha Zanzibar katika kujenga ustawi wa masuala mbali mbali ya maendeleo yao.

Mwenyekiti huyo ameyasema hayo alipozungunza katika mkutano wa hadhara wa chama hiyo huko Bumbwini Makoba ukiwa ni mkutano wa kukamilisha mzunguko wa kwanza wa mikutano ya aina hiyo tokea kuruhusiwa kwa mikutano ya kisiasa miezi  michache iliyopita.

Amesema wazanzibar wanapaswa kuwa wazalendo wa kweli wa nchi yao na kushikamana kwa kuwachana na ugomvi  na uhasama wa wenyewe kwa wenyewe ambao umewachosha sana wanzanzibari kwa kuwa limekuwa likijitokeza kila baada ya uchaguzi.

Amefahamisha kwamba ni  vizuri wazanzibar washikamane kuendesha nchi yao kwa  kuwa na uwezo na mamlaka ya  kuamua kwa pamoja mambo mbali mbali yanayohusu maendeleo ya nchi yao kwa pamoja.

Akizungunzia suala la maadili ameseama kwamba vijana wengi hivi sasa hawana maadili na hivyo wamekosa  mwelekeo   jambo ambalo linahitaji wananchi kuungana nguvu zao kwa pamoja katika kuwasaidia vijana kuwa na mwelekeo utakaosaidia kuchangia vyema ujenzi wa nchi yao. 

Naye Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, amesema kwamba Baraza la Wawakilishi la Zanzibar ni ngome ya wazanzibari na kwamba serikali inawajibu wa kusimamia masuala yanayoamuliwa na kusimamiwa na chombo hicho kwa niaba ya wananchi.

Akizungunzia suala la Muungano amesema kwamba sheria inayopitishwa Zanzibar kuhusu masuala ya Muungano kwa mujibu wa Ibara ya 64 ya Katiba ya Jamhuri sheria hiyo huwa ni batili.

Amefahamisha kwamba mnasaba huo Sheria ya kuyaondoa mafuta na gesi asilia katika orodha ya Mungano kuruhusu utafutaji wa uchimbaji wa mafuta na gesi asilia Zanzibar haiwezi kuwa sahihi kwa vile inapingana na katiba ya Jamhuri.

Amewataka wananchi kukiunga mkono chama hicho na kushikamana pamoja katika kuhakikisha kwamba kwa pamoja wananchi na viongozi wanaitetea Zanzibar kupoata msalahi na haki zake mbali mbali ndani ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Naye Mwenyekiti wa Ngome ya Wanawake wa Chama hicho Taifa Pavu Abdalla Juma , amesema kwamba wananchi wa Bumbwini hawapingani na uamuzi wa serikali wa kuwepo uwekezaji katika ujenzi wa Bandari na shughuli nyengine za maendeleo, lakini inahitaji  watendewe haki kwa  malipo ya  ardhi na vipando vyao kwa thamani halisi ya uwekezaji huo.

Amesema kwamba wananchi wengi walioathirika na mradi huo wamelipwa malipo kidogo jambo ambalo limeleta manunguniko kwa vile malipo waliyopata hayaendani na thamani ya ardhi na vipando vilivyoathirika.

Ameitaka serikali kukaa pamoja na wananchi wa kijiji hicho kutafuta namna bora ya kuondosha manunguniko ya suala hilo ikiwa ni pamoja na kutumia utaratibu wa wananchi kukodisha ardhi zao ili wanufaike zaidi kuliko ilivyo sasa.

Amesema kwamba hakuna sababu wananchi kuchukuliwa aradhi na kulipwa malipo duni ingawa suala la uwekezaji linaungwa mkono na watu wote, lakini alisisitiza kwamba linahitaji kuwa na neema zaidi kuliko kuleta manunguniko.

 Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar

6, Agosti , 2023.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.