Habari za Punde

Gharama za kambi kikwazo kwa wasiojiweza

Mwalimu M kuu Skuli ya Fujoni Abdu Maulid Fidia akiuongoza Uongozi wa Taasisi ya Korea Culture Foundation for Zanzibar (KCFZ) kukagua changamoto za Skuli hiyo ikiwemo uhaba wa Kompyuta.
Mwalimu M kuu wa Skuli ya Fujoni Abdu Maulid Fidia akizungumza na Mkurugenzi wa Taasisi ya Korea Culture Foundation for Zanzibar (KCFZ) Master Kim kuhusiana na uhaba wa Kompyuta  wakati wakiangalia changamoto katika Skuli hiyo
Rais wa  Taasisi ya Maleria Education Foundation (MEF) James park akimkabidhi vyandarua Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Fujoni Abdu Maulid Fidia  kwaajili ya  Wanafunzi wanaokaa kambi ya masomo  Skulini hapo.

Wanafunzi wanaokaa kambi ya masomo wa  Skuli ya Sekondari Fujoni wakiwa katika picha ya  pamoja mara baada ya kukabidhiwa msaada wa vyandarua kutoka kwa Taasisi ya Maleria Education Foundation (MEF).

PICHA NA FAUZIA MUSSA


Na Fauzia Mussa    Maelezo Zanzibar 

 

Wadau wa elimu,wafadhili  na wahisani  wameombwa kujitokeza kusaidia Wanafunzi wanaokaa kambi za masomo kwa ajili ya Maandalizi ya mitihani ya Taifa ili kuunga mkono  Juhudi za Walimu katika  kuhakikisha Wanafunzi hao wanafaulu na kupata matokeo Bora.

 

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada wa chakula na vyandarua kutoka kwa TAASISI ya Corea Culture Foundation for Zanzibar Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Fujoni Abdu Maulid Fidia amesema wanafunzi wengi wanashindwa kushiriki katika kambi hizo kutokana na Hali duni  za maisha yao. 

 

Alifahamisha kuwa jumla ya Wanafunzi 120 wanaotarajiwa kufanya mitihani katika  Skuli ya Fujoni wamekosa fursa ya kushiriki katika kambi hizo  kutokana na kutokumudu gharama za kujikimu hali inayopelekea wanafunzi hao  kukosa fursa ya  kushirikiana na wanafunzi wenzao katika masomo ya ziada.

 

"Tuna jumla ya wanafunzi 198 wanaotarajiwa kufanya mitihani ya taifa kwa mwaka huu,ni wanafunzi 68 tu ndio waliopo kambini hii ni kutokana na familia zao kutokua na uwezo wa kulipia gharama za kambi."alifahamisha

 

Alifafanua kuwa  Kila mwanafunzi  analazimika kulipia laki mbili na hamsini kwa ajili ya mahitaji ya chakula kuanzia mlo wa asubuhi hadi usiku kwa kipindi chote atakachokuwepo kambini ,hivyo msaada wa chakula kutoka kwa wadau na wahisani utawasaidia wale ambao hawamudu gharama za kambi kuweza kushiriki.

 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TAASISI ya Corea Culture Foundation for Zanzibar (KCFZ) Master Kim amesema Lengo la  msaada huo ni kuwasaidia wanafunzi hao kujikimu katika mahitaji  ya chakula na kulinda Afya zao dhidi ya maleria.

 

Aidha alifahamisha kuwa  TAASISI hiyo mbali na  kufundisha utamaduni wa korea kupitia michezo lakini pia imekuwa ikisaidia masuala mbali mbali ya  kijamii ikiwemo kutoa msada wa vyakula na kuchimba visima vya maji katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar.

 

Mapema Wanafunnzi wa Skuli ya Fujoni waliishukuru  TAASISI hiyo  Zanzibar Kwa msaada huo na kuwataka kuendeleza kutoa misaada kama hiyo mara kwamara kwani chakula ni kitu kinachohitajika na kutumika katika maisha ya Kila siku.

 

Walisema endapo wadau na wahisani watatoa msaada wa chakula katika kambini kutasaidia walioshindwa kumudu gharama za kujikimu kuweza kushiriki masomo katika kambi hizo.

"Mazingira ya Fujoni yanazalisha mbu Sana tunashukuru Kwa msaada huu wa vyandarua utatuwezesha kusoma kwa amani na kutukinga Sisi na maambukizi ya malaria"walifahamisha wanafunzi hao


Wakati huo huo watendaji wa TAASISI ya Korea Culture Foundation for Zanzibar walitembelea eneo wanaotarajiwa kuwekeza Chuo cha michezo katika kijiji cha Fujoni mara utaratibu utakapokamilika.

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.