RAIS wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amewataka wahitimu wa vyuo vikuu
kutumia elimu zao, kuchangia Maendeleo ya nchi kwa nafasi mbalimbali za taaluma
zao.
Dk. Mwinyi aliyasema
hayo, kwenye mahafali ya 21 ya Chuo Kikuu cha Zanzibar (ZU) Tunguu, Wilaya ya
Kati Mkoa wa Kusini, Unguja.
Alisema, Elimu ni
ajenda muhimu kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM, 2020 - 2025, yenye lengo la
kuongeza kasi ya maendeleo kwa taifa na wananchi wake.
Alisema nguvu kazi
yenye elimu bora na maarifa ina mchango muhimu kwa maendeleo ya kila sekta.
Halkadhalika, Rais
Dk. Mwinyi alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, awamu ya nane imejikita
zaidi kuleta mageuzi makubwa kwenye sekta ya elimu ikiwa ni kipaombele chake, kwa
kuzifanyia kazi changamoto zinazotokana na sekta hiyo ikiwemo kuboresha maendeleo
na miundombinu ya kisasa, kuimarisha vifaa vya kufundishia, maabara, maktaba,
vyumba vya kompya, vyoo na mazingira mazuri ya walimu katika kuchochea mageuzi
na maendeleo ya kiuchumi wa Zanzibar.
Aidha, Rais Dk.
Mwinyi alieleza, uhusuano na ushirikiano uliopo baina ya Serkali ya
Mapinduzi ya Zanzibar na Taasisi ya elimu ya juu vikiwemo vyuo vikuu ya umma na
binafsi, vina mchango muhimu kuhakikisha Zanzibar inatoa elimu bora na
kuchochea maendeleo kwa kada zote.
Alieleza vyuo vikuu
na taasisi nyengine za elimu Zanzibar, vinafanya kazi nzuri ya kuwaandaa
wataalamu wakushika nafasi mbalimbali za utumishi Serikalini na taasisi binafsi.
Akizuzungumzia maendeleo
kwenye Sekta ya Afya, Rais Dk. Mwinyi amesema Serikali pia imeweka mkazo zaidi
kuimaisha miundominu ya kisasa kwenye hospitali zote za Serikali kwa kufanya
mageuzi makubwa ikiwemo kuboresha miundominu ya kisasa ya matibabu kwa hospitali
zote za Wilaya Unguja na Pemba pamoja na kuangalia upya sera ya afya mifumo ya
utoaji huduma za afya.
Pia Dk. Mwinyi, alikipongeza
Chuo kikuu cha Zanzibar kwa kuanzisha shahada ya Sayansi ya afya ya jamii na
kukiahidi chuo hicho kupata ushirikiano zaidi kutoka kwa serikali ili
kuhakikisha lengo la kuanzishwa fani hiyo linafanikiwa sambamba na kukitaka
chuo hicho kubuni fani zenye mahitaji ya soko la ajira nchini pamoja na mipango
ya maendeleo.
Aidha, aliwataka
wahitimu hao kuangalia fursa zilizopo kwa nia ya kuongeza viwango vyao vya
elimu. Samamba na kuwataka wageni waliopo nchini kutenga muda wa kuangalia
vivutio vya Utalii vilivyomo nchini ikiwemo hifadhi ya Mji Mkongwe wa Zanzibar,
fukwe, mashamba ya viungo, pamoja na sehemu za historia ili wakawe mabalozi wazuri
wa kuisifia Zanzibar watakaporejea nchini mwao.
Naye, Waziri wa Elimu
na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Muhammed Mussa alikitaka chuo Kikuu cha
Zanzibar (ZU) kuongeza wigo kwenye fani za sayansi hasa kwa kada za udaktari na
ufamasia ili kukuza vipaji vilivyoandaliwa tokea ngazi za maandalizi, msingi na
sekondari.
Akizungumza kwenye
Mahafali hayo, Mkuu wa Chuo hicho, Dk. Abdul Kadir Othman Hafidh aliipongeza
juhudi zinazofanywa na Rais Dk. Mwinyi katika kuharakisha maendeleo ya nchi
kupitia sekta ya Elimu Zanzibar, hasa kuimarisha miundombinu ya kisasa inayotoa
hamasa kwa wanafunzi kujisomea.
Mwenyekiti wa Baraza
la Chuo hicho, Juma Burhan Mohamed ambae pia ni Mkurugenzi mtendaji, Wakala wa Uwezeshaji
wananchi Kiuchumi, aliwataka wahitimu hao kutembelea ofisi za uwezeshaji ili
kujifunza kivitendo na kuangalia fursa za masoko ya ndani na nje na kujifunza
jinsi ya kujitegemea.
IDARA YA
MAWASILIANO IKULU, ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment