Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dk. Hussein Ali
Mwinyi ameahidi kuendeleza ushirikiano mwema kwa wananchi wa
kijiji cha Bweleo na kufuata nyayo za Marehemu Mzee Ali Hassan Mwinyi.
Alhaj Dk. Mwinyi pia aliwaahidi
wananchi hao kuyabeba na kuwa wajibu wake kwa yote yaliyokuwa yakitekelezwa na
Marehemu Mzee Mwinyi kijijini hapo.
Al hajj Dk. Mwinyi, ametoa ahadi hizo
kwenye Kijiji cha Bweleo Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi, mara
baada ya ibada ya sala ya Ijumaa iliyofuatiwa na du’a maalum ya kumuombea Marehemu
Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais mstaafu wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania aliefariki dunia Mwezi Februari mwaka huu.
Pia, Al hajj Dk. Mwinyi
aliwashukuru wanakijiji hao na Watanzania kwa ujumla kwa kuendelea muombea du’a
njema mzee wao.
Akisoma risala kwenye ibada hiyo, kwa
niaba ya wanakijiji cha Bweleo Maalim, Khamis Mussa ambae pia ni kiongozi wa
Msikiti wa kijijini hapo, alimuomba Alhaj Rais Dk. Mwinyi na familia ya Hayati
Mzee Mwinyi kwa ujumla kuendeleza ushirikiano aliouwacha Mzee wao kijijini hapo
kwenye masuala mbalimbali ya jamii.
Aidha, walishikuru mambo
makubwa mawili aliyofanya Mzee Ali Hassan Mwinyi kijiji hicho na sasa yamewaletea heshima kubwa
kwao ikiwemo kuwapa maeneo mawili likiwemo Jengo la vijana wa
Bweleo na shaba kubwa la kinamama ambayo aliyasimamia vyema hadi aliyapatia warka nasasa wanabweleo
wanayamiki kisheria.
Alisema maeneo hayo kwasasa Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar imeyaboresha kwa kujenda Chuo Cha Mafunzo
ya Amali chenye tija kubwa kwa Wanabweleo na nchi kwa ujumla pia Samba la miti
la Ushirika wa kina mama kwasasa Serikali inalijenga Chuo chenye hadhi na jina
kubwa duniani Chuo cha IIT Madrsa ikiwa ni tawi la chuo hicho kutoka India
ambacho kimeipatia Bweleo, Zanzibar na Tanzania kwa ujumla, heshima kubwa ndani
na nje ya nchi.
Mbali na mambo mengine pia wanakijiji
hao wameiomba Familia ya Marehemu Mzee Mwinyi kuendelea kuyashikilia masuala ya
jamii yaliomo kijijini humo ikiwemo maulidi na dhkri za kila mwaka sambamba na
kuwatembelea wazee na wanajamii hao.
Pia wanakijiji hao waliishukuru falimia
ya Mzee Mwinyi kwa kuiheshimisha Bweleo siku ya Msiba wa Mzee Mwinyi kwa Mwili
wake kulazwa kijijini hapo nakuthimulia mwaka 1984, alipokua Rais wa Zanzibar, Mzee Ali Hassan Mwinyi
alifanya ziara ya kwanza kijijini hapo na kuweka historia na heshima kubwa ya
kijiji chao kwa nyakati zote za uongozi wake akiwa mkuu wa nchi.
Mapema akikhutubu kabla ya sala ya Ijumaa,
Khatib Sheikh, Mussa Ali Kirobo aligusia suala la Hijja na vipaombele
vilivyoombwa na baadhi ya taasisi za hijja nchini kwa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, ikiwemo ombi la uwepo wa usafiri wa Moja kwa moja kutoka Zanzibar
hadi Makkah Saudi Arabia, kuboreshwa kwa mfumo wa hijja visiwahi ili kutoa
fursa kubwa ya Mahojji wengi Kwenda kutekeleza ibada hiyo ikiwemo pendekezo la
kuanzishwa kwa hesabu maalumu za benki (account) kwa kila mtoto atakayezaliwa
kuanzishiwa ili akiwa na uelewe kuwepo wepesi na nafasi nyingi za watu Kwenda
kuhiji akitolea mfano nchi ya Indonesia iliopo bara Asia ambao hufuata mfumo
huo.
Aidha, Khatibu huyo aliishauri Serikali kuangalia uwezekano
wa kuanzishwa kwa utalii wa kiislamu kwa kutoa fursa ulimwenguni kote kuja
kuizuru Zanzibar kwa masuala ya dini badala ya utalii wa kawaida pekee iki
kuzidi kuijengea sifa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR.
No comments:
Post a Comment