Habari za Punde

SERIKALI YAONGOZA MAZISHI YA ALIYESHIRIKI TUKIO LA KUCHANGANYA UDONGO

 

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis akitia saini kitabu cha maombolezo alipowasili nyumbani kwa Marehemu Mzee Hasanieli Mrema aliyeshiriki katika tukio la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar, mazishi yaliyofanyika katika Kijiji cha Midawi, Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Serikali imesema itaendelea kuuthamini na kuuenzi mchango wa wazee walioshiriki katika tukio la kihistoria la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis wakati akitoa salamu za Serikali katika mazishi ya Mzee Hasanieli Mrema aliyeshiriki katika tukio la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar, katika Kijiji cha Midawi Midawi, Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro leo tarehe 08 Mei, 2024.

Amesema Marehemu Mzee Mrema ambaye wakati alishiriki tukio hilo muhimu akiwa kijana wa umri wa miaka 20 akiwa na wenzake tarehe 26 Aprili, 1965 katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam mwaka mmoja baada ya Muungano enzi za uhai wake alikuwa tayari kuzungumzia faida za Muungano huo.

 Wengine watatu walioshiriki tukio hilo la kuchanganya udongo ni Mzee Hassan Omari Mzee kutoka Zanzibar, Marehemu Bi. Khadija Abasi Rashid kutoka Zanzibar na Bi. Sifael Mushi kutoka Tanzania Bara.

Naibu Waziri Khamis amesema marehemu alitoa wito kwa Watanzania hususan vijana kuulinda na kuutetea Muungano na hata alipoombwa kuhojiwa na waandishi wa habari, hakusita kufanya hivyo.

Mhe. Khamis ameungana na waombolezaji kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu ambapo amewasilisha salamu za pole kutoka kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango.

 Mhe. Khamis amesema marehemu alishiriki katika Kongamano la Kitaifa la miaka 58 ya Muungano lililofanyika Dodoma tarehe 26 Aprili, 2022 ambalo liliambatana na uzinduzi wa Kitabu cha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Chimbuko, Misingi na Maendeleo, katika tukio hili wenzake watatu hawakuweza kushiriki kutokana na changamoto za kiafya.

“Tunamshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa maisha yake na tutazikumbuka nyakati zote ambazo tuliweza kushiriki naye katika matukio muhimu ya kitaifa hususan sherehe za Muungano ambapo yeye na wenzake watatu (Mzee Hassan, Bi. Sifael na Marehemu Bi. Khadija) walishiriki kwa pamoja katika sherehe za Muungano zilizofanyika Tanzania Bara (Dar es Salaam na Dodoma) na Zanzibar pia,“ amesema Mhe. Khamis.

Naibu Waziri Khamis ametoa rambirambi kwa familia ya marehemu kwa niaba ya Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Mpango na kusema kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu awape ngvu na ustahimiloivu katika kipindi hiki kigumu.

 Shughuli hiyo ya mazishi hayo imehudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Moshi Zephania Sumaye kwa aliyemwakilisjha Mkuu wa Kilimanjaro, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Cesilia Nkwamu na viongozi wa wilaya.




Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis akiungana na viongozi mbalimbali wa wilaya na waombolezaji katika katika mazishi ya Marehemu Mzee Hasanieli Mrema aliyeshiriki katika tukio la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar, mazishi yaliyofanyika katika Midawi, Old Moshi mkoani Kilimanjaro 
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis akitoa salamu za Serikali wakati wa mazishi ya Marehemu Mzee Hasanieli Mrema aliyeshiriki katika tukio la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar, mazishi yaliyofanyika katika Midawi, Old Moshi mkoani Kilimanjaro
Mkuu wa Wilaya ya Moshi Zephania Sumaye akitoa salamu za Mkoa wakati wa mazishi ya Marehemu Mzee Hasanieli Mrema aliyeshiriki katika tukio la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar, mazishi yaliyofanyika katika Midawi, Old Moshi mkoani Kilimanjaro 
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Mzee Hasanieli Mrema aliyeshiriki katika tukio la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar, mazishi yaliyofanyika katika Midawi, Old Moshi mkoani Kilimanjaro 
Sehemu ya waombolezaji wakiwa katika mazisihi ya Marehemu Mzee Hasanieli Mrema aliyeshiriki katika tukio la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar, mazishi yaliyofanyika katika Midawi, Old Moshi mkoani Kilimanjaro 

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis akiweka shada la maua katika kaburi la Marehemu Mzee Hasanieli Mrema aliyeshiriki katika tukio la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar, mazishi yaliyofanyika katika Midawi, Old Moshi mkoani Kilimanjaro.

Sehemu ya waombolezaji wakiwa katika mazisihi ya Marehemu Mzee Hasanieli Mrema aliyeshiriki katika tukio la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar, mazishi yaliyofanyika katika Midawi, Old Moshi mkoani Kilimanjaro leo tarehe o8 Mei, 2024.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.