Mkoa wa Mjini Mgharib Na. Mwandishi OMKR.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema ni muhimu kwa jamii kushikamana na
tabia za watu wema kwa kuwa ni maagizo kutoka kwa Mwenyezimungu muumba, katika
kufikia kupatikana daraja kubwa za kheri kwa duania na akhera.
Mhe. Othman ameyasema hayo huko
Kiponda mjini Zanzibar alipotoa salaam kwa waumini wa dini ya kiislamu
waliohudhuria katika khitima ya kumuombea dua marehemu Mohammed Raza ambaye
jana ametimiza mwaka mmoja tokea alipofariki dunia.
Amesema watu wema bila kujali
kipato walichonacho ama darja yao katika jamii au nyadhifa za siasa
wanajishusha kwa nia ya kujiweka pamoja na jamii sambamba na kuwasaidia wenzao
kwa kila walichoruzukiwa na mwenyezimungu kwa kuwa ndio njia mojawapo muhimu ya
kutekeleza ibada.
Alisema tabia za Marehemu Raza
zilijeweka katika akhalaki njema kwa kuishi na watu kwa amani na kwasaidia
wengi bila kujali ikiwa ni pamoja na kuishi nao kwa kuchanganyika na jamii zote
katika mazingira tofauti licha kwamba mungu alimruzuku wasaa mkuwa
wa kipato kuliko walivyowengi.
Amesema kwamba iwapo jamii
itashikamana na kuishi katika hali kama hiyo ya kushikamana na tabia njema ya
kumjali kila mmoja ni elimu na darsa kubwa kwa waumini na ni hatua ya
kujijengea khatima njema katika kupata malipo mema ya akhera kutoka kwa mola
muuumba.
Mhe. Makamu amesema kwamba watu
wenye tabia njema wametukuzwa na mwenyezimungu ikiwa ni pamoja na kuwa na
watoto wenye kuwaombea dua wazazi wao
waliotangulia mbele ya haki ili kuendeleza mema yao waliyoyaacha na
ujira wao kutoka kwa mungu uweze kuendelea.
Amefahamisha kwamba hali hiyo sio
tu kwamba huleta furaha kwa wanajami lakini pia husaidia nchi kuwa na Amani na
kuwepo mshaikamano wa umma katika kuleta maendeleo ya taifa lao na kwamba Raza
alijitaihdi kuwa pamoja na watu.
Amesema kwamba marehemu Raza pamoja
na kuwa na mali nyingi, lakini aliishi katika maisha ya maagizo ya vitabu
vitakatifu kwa kutokushughulishwa sana na mali hiyo na badala yake alifanya mengi ya kusaidia kama
ujenzi wa misikiti , madrasa na vituo vya afya jambo lililomfanya kuweka alama
njema katika kupeleka mbele dini kwenye maeneo mengi ya visiwa vya Unguja na
Pemba.
Naye Mhadhiri wa kimatiafa katika
mihadhara ya Kiislamu kutoka Landon Sayyed Ammar amesema kwamba alichofanya Marehemu Raza ni kuweka Uzanzibari
wake mbele kwa kuipenda nchi yake na kufanya hivyo ni kutekeleza ibada kupitia
nguzo ya imani jambo ambalo linahitaji kufanywa na waumini wote.
Akitoa shukran kwa niaba ya
waliohudhuria kwenye dua hiyo Mshauri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania wa mambo ya siasa Mhe. Haji Omar Kheir, alishauri wanafamilia
kushirikiana na wataalamu mbali mbali kuyaandikia kitabu mema yote aliyoyafanya
marehemu Raza.
Naye Mtoto Mkubwa wa Marehemu Hassan Raza, akitoa shukrani kwa niaba ya familia amewashururu viongozi , wananchi na watu mbali mbali kwa kuwa pamoja katika kumuombea dua marehemu baba yao na kueleza kwamba katika kuendeleza mambo mema aliyokuwa akiyafanya baba yao wapo kwenye hatua za mwisho kusajili fondesheni ya kuweka kielelezo cha kumuenzi mzee wao huyo.
Mwisho.
Kitengo cha Habari.
Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais
wa Zanzibar
Juni, 09.06.04.
No comments:
Post a Comment