Habari za Punde

WAZIRI WA HABARI VIJANA UTAMADUNI NA MICHEZO TABIA MAULID MWITA AFANYA ZIARA KUANGALIA UJENZI WA JENGO LA SHIRIKA LA MAGAZETI YA SERIKALI TUNGUU ZANZIBAR.

Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Mh,Tabia Maulid Mwita akipatiwa maelezo  na Mshauri Elekezi kutoka Wakala wa Majengo Zanzibar Abubakar Mohamed Bakari  wakati akiangalia Ramani ya Ujenzi katika ziara maalum kutembelea Ujenzi wa Jengo litakalokua  Shirika la Magazeti ya Serikali Tunguu Wilaya ya Kati Unguja
Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Mh,Tabia Maulid Mwita akifahamisha kitu kwa Wakandarasi wakati akitembelea sehemu mbalimbali za Jengo akiwa katika  ziara maalum kutembelea Ujenzi wa Jengo litakalokuwa  Shirika la Magazeti ya  Serikali Zanzibar Leo   Tunguu Wilaya ya Kati Unguja.

Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Mh,Tabia Maulid Mwita akifahamisha kitu kwa Wakandarasi wakati alipofanya ziara maalum kutembelea Ujenzi wa Jengo litakalokua  Shirika la Magazeti ya Serikali  Zanzibar Leo   Wilaya ya Kati Unguja.

Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Mh,Tabia Maulid Mwita (katikati)akipatiwa maelezo kuhusu Jengo na Mshauri Elekezi kutoka Wakala wa Majengo Zanzibar Abubakar Mohamed Bakari wakati alipofanya ziara maalum kutembelea Ujenzi wa Jengo la Shirika la Magazeti ya Serikali Zanzibar Leo Tunguu Wilaya ya Kati Unguja.

Na Khadija Khamis- Maelezo . 20/07/2024.

Waziri wa Habari, Vijana ,Utamaduni na Michezo Mhe. Tabia Maulid Mwita amewataka  Wakandarasi wa mradi wa Ujenzi wa Jengo la Shirika la Magazeti (Zanzibar leo) kusimamia matakwa  yaliyomo kwenye mkataba ili kufanya kazi kwa ufanisi.

Ameyasema hayo huko Tunguu Wilaya ya Kati Unguja wakati alipofanya ziara ya kukagua maendeleo na hatua zilizofikia za ujenzi huo.  

Amesema mradi huo umeshafikia asilimia 30 hadi sasa na kuishajihisha Kampuni ya ujenzi huo Skyward Construction kumaliza kabda ya muda ulioweka kutokana na hatua, spidi pamoja na uwezo wa Kampuni hiyo .

“Nakushajihisheni  kuwa pamoja na kwamba mkataba umesema ujenzi utamalizika  mwezi wa tisa 2025,nakuombeni mufanye kazi kwa spidi tumalize  kabla ya muda  huo .”amesema Waziri Tabia .

Waziri Tabia alimtaka Mhariri Mtendaji  wa Shirika la Magazeti Ali Haji Mwadini kuwa karibu na  Wakandarasi ili kuweza kutatua changamoto kwa haraka  pindipo zikijitokeza .

Akitoa wito kwa wananchi wanaoishi katika maeneo hayo amewaomba kutoa mashirikiano kwa wakandarasi ili kufanikisha mradi huo kwa wakati uliopangwa .

Nae Mhariri Mtendaji wa Shirika la Magazeti Zanzibar Ali Haji Mwadini amesema utapokamilika  ujenzi huo utaleta ufanisi mkubwa katika Shirika hilo jambo ambalo litatoa fursa ya kutumia mitambo yake wenyewe ya kutengenezea  magazeti .

Sambamba na hayo jumla ya familia nane za watumishi wa shirika hilo watapatiwa nyumba za kuishi katika eneo hilo  jambo ambalo litasaidia kuongeza ufanisi .

Amefafanua  kuwa mradi huo utajumuisha Jengo la Ghorofa nne, Nyumba za Watumishi zitakuwa na ghorofa  moja,  ambazo zitachukuwa familia nane, Kiwanda cha Magazeti , pamoja na Msikiti  

Kwa upande wa Mshauri elekezi wa Wakala wa Majengo Abubakar Mohamed Bakari ameahidi kusimamia ujenzi huo na kuhakikisha unamaliza kwa muda muafaka na kiwango kilichokusudiwa .

Jumla ya Shilingi Billion 8.1, 2 zitatumika kwa utekelezaji wa mradi huo ambao umeanza kutekelezwa mnamo  Mwezi Machi mwaka 2024 na kutarajiwa kumalizika Septemba 2025.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.