6/recent/ticker-posts

Uzinduzi wa Gari la Mtambo wa Kukagua Makontena Bandarini.

Gari Maalum lenye Mashine ya kukagua Makontena yanayoingia Nchina na Bidhaa mbalimbali huweza kukaguliwa bila ya kuyafungua ndani na kutumia Mtambo huu kukagua kupitia Scana na kuona kila kitu kiliomo ndani ya kuntena na kuweza kulipia Ushuru bila ya kudanganya na kuiongezea Serekali mapato na kupunguza Msongamano wa Makontena katika bandari ya Zanzibar.
Kontena likikaguliwa wakatika wa Makabidhiano ya Mtambo huo na Balozi Mdogo wa China Zanzibar Xie Yun Liang, katika viwanja vya Ofisi ya TRA Mlandege Zanzibar.
Waziri wa Fedha wa Zanzibar Omar Yussuf Mzee, akihutubia wakati wa sherehe za kukabidhiwa Gari Maalum laMtambo wa Kukagua Makontena Bandarini kutoka Serekali ya China, makabidhiano hayo yamefanyika katika Ofisi za TRA Mlandege Zanzibar.

Balozi Mdogo wa China Zanzibar Xie Yun Liang, akizungumza wakati wa kukabidhi Gari Maalum la kukagulia makontena yanaoingia katika Bandari ya Zanzibar,  
 NAIBU Kamishna wa TRA Zanzibar Mcha Hassan, akizungumza katika sherehe hizo za uzinduzi wa gari maalum yenye mashine ya kukagulia makontena bandari ili kupata thamani halisi ya mzingo uliokuwemwe ndani ya kontena.
 MAOFISA wa  TRA Zanzibar wakiangalia  kabrasha la picha zinazoonesha utendaji wa kazi za Mtambo Maalum wa kuchunguza Makontena katika Bandari ya Zanzibar ili kudhibiti uhalali wa kulipia Ushuru wa Forodha kwa mizigio inayoingia Zanzibar kutoka nje ya Nchi.

 Maofisa wa Ubalozi wa China na kutoka katika kampuni iliotengeneza mashine hiyo wakimsikiliza Waziri wa Fedha Zanzibar akihutubia katika sherehe za makabidhiano ya Mtambo huo wa kukagua Makontena Bandarini. Sherehe hizo zimefanyika katika viwanja vya TRA Mabluu .
 WAZIRI wa Fedha Zanzibar Omar Yussuf Mzee, na Balozi Mdogo wa China Zanzibar, Xie Yun Liang, wakitiliana saini makabidhiano ya Gari lenye mtambo wa kukagulia makontena  yanayoingia Zanzibar kupitia bandari ya Malindi, mtambo huo una uwezo wa kumurika kili kitunkilimo katika kontena na kupata thamani hali ya mzingo uliokuwemo katika kontena hilo.
Balozi Mdogo wa China Zanzibar  Xie Yun Liang, akizungumza na Waziri wa Fedha Zanzibar Omar Yussuf Mzee, wakati wa uzinduzi wa gari la Mitambo ya Kukagulia Kontena Bandarini, akitowa maelezi jinsi linavyofanya kazi gari hilo wakati wa makabidhiano yaliofanyika Ofisi za TRA Zanzibar.
WAFANYABIASHARA   wa Zanzibar wakishuhudia  uzinduzi wa Gari maalumu yenye mtambo wa kukagua makontena bandari wakiwa nje ya viwanja vya TRA Mabluu.

 
 

Post a Comment

1 Comments

  1. Kwa TRA hii iliyojaa mijizi. Wakiona hilo gari linawaletea noma kuendeleza kuiba wataliharibu kesho tu. Suala sio kua na teknolojia za kisasa Mh. Suala la msingi ni kudhibiti wizi mkubwa kwenye idara hii.

    ReplyDelete