Habari za Punde

Askofu Laizer kuzikwa Ijumaa



Joseph Ngilisho,Arusha
ASKOFU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini kati,marehemu Askofu Dk. Thomas Laizer atazikwa siku ya Ijumaa katika kanisa kuu la KKKT.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamati ya mazishi  na familia ya marehemu, iimeeleza kuwa marehemu atazikwa katika  kanisa hilo lililopo  mjini kati Arusha,kama ishara ya kuwaenzi maaskofu wa
kanisa hilo ,tofauti na awali ambapo taarifa zilidai angezikwa nyumbani kwake.

Aidha taarifa hiyo imesema kuwa waumini na washirika wa kanisa kuu na makanisa yote ya KKKT nchini, wananchi, ndugu jamaa na marafiki
watapata fursa ya kutoa heshima zao za  mwisho kwa mwili wa marehemu kuanzia siku ya Alhamisi mchana.

Taarifa hiyo iliongeza kuwa mwili wa Askofu Laizer utalala kanisani hapo hadi Ijumaa kwa mazishi.


Marehemu Askofu Laizer aliyezaliwa Machi 10, 1945 katika kijiji cha Kitumbeine wilayani Longido  na baade kupata elimu yake ya msingi hadi darasa la nane Longido na kumaliza mwaka 1965.

Askofu Laizer, aliendelea na masomo yake ya juu ndani na baade kujiunga na masomo ya Theolojia katika chuo cha Makumira na baade kuongeza masomo nchini Marekani.

Marehemu wakati wa uhai wake alikuwa Mwinjilisti na mchungaji katika makinisa mbalimbali nchini na baade kuwa Mkuu wa jimbo na Mkuu wa Sinodi na baade kuwa Rais wa Sinodi kabla ya kupandishwa cheo kuwa Askofu wa kwanza wa Dayosisi ya Arusha ambayo kwa sasa ni Dayosisi ya Kaskazini Kati.

Mazishi ya Askofu Laizer yanatarajiwa kuhudhuriwa na idadi kubwa ya watu kutoka maeneo mbalimbali nje na ndani ya nchi, huku viongozi wa serikali wakitarajiwa kuongoza mazishi hayo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.