Habari za Punde

Ligi ya Mpira wa Kikapu Zanlink Kanda ya Unguja kati ya Stone Town na Rangers.


Kikosi cha timu ya Stone Town kilochotoka na ushindi wa Vikapu 57 kwa 43 dhidi ya timu ya Rangers katika mchezo wa ufunguzi wa Ligi ya Zanlink Kanda ya Unguja mchezo uliofanyika uwanja wa maisara.
Kikosi cha timu ya Mpira wa Kikapu Zanzibar Rangers wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mchezo wao wa ufunguzi wa Ligi ya Kikapu Zanlik Kanda ya Unguja, ilikubali kipigo cha Vikapu 57-43. 
Afisa wa Kampuni ya Zanlik, Ndg Nasibu Amour akikagua timu ya Kikapu ya Rangers wakati wa mchezo wa ufunguzi wa Ligi hiyo ikiwa chini ya Udhamini wa Kampuni ya Mtandao wa Intenet unaotolewa na Zanlink Zanzibar. 
Afisa wa Kampuni ya Zanlink, Ndg Nasibu Amour akiwa na maofisa wa Kampuni ya Zanlink , Ndg Burhan Miraji na Winnie Rongoma e  wakikagua timu ya Kikapu ya Stone Town,wakati wa mchezo wa ufunguzi wa Ligi hiyo ikiwa chini ya Udhamini wa Kampuni ya Mtandao wa Intenet unaotolewa na Zanlink Zanzibar. 
Wachezaji wa Stone Town na Rangers wakiwania mpira wakati wa kuaza kwa mchezo wao wa ufunguzi wa Ligi ya Mpira wa Kikapu Zanlink Kanda ya Unguja, uliofanyika uwanja wa maisara timu ya Stonev Town imeshinda kwa vikapu 57-43.  

Mchezaji wa Timu ya Stone Town Dulla Zungu akiwa na mpira wakati wa mchezo wao wa ufunguzi wa ligi mpira wa Kikapu Kanda ya Unguja, uliofanyika katika viwanja vya maisara Zanzibar timu ya Stone Town imeshinda kwa vikapu 57--43 
Wachezaji wa timu ya Stone Town na Rangers wakiwania mpira wakati wa mchezo wao wa ligi ya Kikapu Kanda ya Unguja.
 








No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.