Habari za Punde

Balozi Seif Aungana na Wananchi katika Maziko ya Mmoja wa Marehemu waliopata ajali jana.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Balozi Seif Ali Iddi wa Sita kutoka kushoto akijumuika pamoja na waumini wa dini ya Kiislamu katika kumsalia Marehemu Mwanahawa Ali Machano aliyekuwa Mwenyekiti wa UWT Tawi la Shauri Moyo Mjini Zanzibar.Kulia ya Balozi Seif ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kaskazini Unguja Nd. Haji Juma Haji.
Marehemu Mwanahawa aliyezikwa kijijini kwao Uyagu Mkwajuni Mkoa wa Kaskazini Unguja alikuwa miongoni mwa wanafunzi watatu wa darasa la Itikadi la CCM waliokuwa wakitokea Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja kwa zira za Kimasomo.
Picha na – OMPR – ZNZ.

Na Othman Khamis OMPR.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi Balozi Seif Ali Iddi leo alijumuika pamoja na wana CCM, Wananchi pamoja na Wana Familia katika Mazishi ya Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania        { UWT } Tawi la Shauri Moyo Bibi Mwanahawa Ali Machano.

Maziko ya Bibi Mwanahawa Ali  aliyefariki Dunia jana jioni kufuatia ajali ya Gari  iliyotokea Mkokotoni Mkoa wa Kaskazini Unguja  yamefanyika kijiji kwao  Uyagu Mkwajuni Wilaya ya Kaskazini “ A “.

Mwenyekiti huyo wa UWT Tawi la Shauri Moyo alikuwa miongoni mwa wanafunzi watau  wa Darasa la Itikadi la Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Amani waliofariki Dunia  wakitokea katika ziara ya kimasomo Nungwi Mkoani humo.

Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo walieleza kwamba Basi lililokuwa likiwasafirisha wanafunzi hao wa Darasa la Itikadi lilipatwa na mtihani huo wakati Dereva wa Gari hiyo alipojaribu kulikwepa Gari la Ng’ombe lililokatisha bara bara ghafla katika maeneo ya karibu na chuo cha Amali Mkokotoni.
Marehemu Mwanahawa Ali Machano ameacha Mume na Watoto sita. 

Mwenyezi Muungu alilaze Roho ya Marehemu mahali pema peponi. Amin.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.