Habari za Punde

Dk Bilal aifariji familia ya Rubani William Slaa


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaini kitabu cha kumbukumbu ya maombolezo kufuatia kifo cha marehemu Rubani William Slaa aliyefariki Dunia wiki iliyopita kwa ajali ya Helikopta wakati Makamu wa Rais alipofika nyumbani kwa Marehemu Slaa  Gongolamboto jijini Dar es salaam leo Octoba 20, 2015. (Picha na OMR)
 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na kumfariji Meya wa Manispa ya Ilala Mhe. Jery Slaa alipofika nyumbani kwao Gongolamboto jijini Dar es salaam leo Octoba 20, 2015 kwa ajili ya kutoa mkono wa pole kufuatia kifo cha Baba yake Marehemu Rubani William Slaa aliyefariki wiki iliyopita kwa ajali ya Helikopta.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.