Habari za Punde

Mgombea wa Urais Kupitias CCM Dk Shein Apokea Wanachama Wapya Kutoka CUF 38, Katika Mkutano wake wa Kampeni Kiungoni Jimbo la Kojani Pemba.

Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Wazee wa Jimbo la Kojani alipowasili katika viwanja vya mpira kiungoni Wilaya ya Wete Pemba kwa kuaza Mkutano wake wa Kampeni kisiwani Pemba.
Kikundi cha Taraab cha Mzee Gogo Kangagani kikitoa burudani katika viwanja vya Mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, katika viwanja vya mpira kiungoni Wilaya ya Wete Pemba.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Wete Pemba Ndg Kombo Hamad Yussuf, akizungumza wakati wa mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk Ali Mohamed Shein uliofanyika katika viwanja vya mpira kiungoni Pemba. 
Wananchama wa CCM Jimbo la Kiungoni Pemba wakifuatilia Mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, uliofanyika katika viwanja hivyo.
Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dk Ali Mohamed Shein, akiwa na Viongozi wa CCM wakimsikiliza Mwenyekiti wa CCM Wilaya Wete wakiti akihutubia katika mkutano huo na kuwataka Wan anchi Kisiwani Pemba kumpigia Kura ya Ndio Dk Shein na Wagombea wote wa CCM. 
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk Ali Mohamed Shein, akimpokea aliyekuwa Mwanachama wa CUF Ndg Rashid Mohammed Hassan,kwa kuamua kujiunga na CCM, na kumkabidhi Kadi yake ya CUF Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, wakati wa mkutano wake wa Kampeni uliofanyika katika viwanja vya kiungoni Wilaya ya Wete Pemba Jumla ya Wanachama wapya 38 wamejiunga na CCM wakitikea CUF.

Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk Ali Mohamed Shein, akimpokea aliyekuwa Mwanachama wa CUF Ndg Khamis Halfan Khamis,kwa kuamua kujiunga na CCM, na kumkabidhi Kadi yake ya CUF Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, wakati wa mkutano wake wa Kampeni uliofanyika katika viwanja vya kiungoni Wilaya ya Wete Pemba Jumla ya Wanachama wapya 38 wamejiunga na CCM wakitikea CUF.










1 comment:

  1. Duu, sikuwahi kuamini kua CCM bado ipo Pemba!!.. kwa muda wote wa ziara ya Dr. Shein huko nashuhudia maajabu!.

    Hii inanifanya nianze kuamini maneno ya rafki yangu mmoja wa kipemba aliewahi kuniambaia kua kufa kwa ccm Pemba, kulisababishwa na baadhi ya "WALAJI" wachache ndani ya chama ambao waliona njia rahisi ya kufaidi madaraka na nafasi za watoto wao ndani ya SMZ ni kuwanasibisha WAPEMBA wote na CUF ili wao peke yao ndio waonekane wazalendo na ccm wa kweli kweli!

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.