Habari za Punde

Kampeni Mazingira Bora Elimu Bora


TAARIFA KWA VYOMBO  VYA HABARI

UTANGULIZI;
Habari  za Asubuhi  ndugu zangu wana habari,
Leo tarehe 17/01/2016,Mimi Bonnah M.Kaluwa ambaye ni mbunge wa jimbo la Segerea katika wilaya ya Ilala.
Nimekuiteni Asubuhi ya leo ili kuwashirikisha katika uzinduzi wetu wa kampeni  ya MAZINGIRA BORA KWA ELIMU BORA  ndani ya jimbo la Segerea,kwakujua  dhahiri kuwa ushiriki wa wana habari ni muhimu sana katika kufanikisha  kampeni  hii kwa ajili ya maendeleo ya elimu katika jimbo la Segerea na nchi kwa ujumla .

MAZINGIRA BORA KWA ELIMU BORA ,ni kampeni isiyo na malengo ya kumnufaisha mtu binafsi bali inalenga kuisaidia jamii ndani ya jimbo la Segerea katika upatikanaji wa elimu bora kupitia maboresho ya  miundombinu  ya shule kama madarasa, vyoo,  mifumo  ya maji safi na salama, madawati na kadhalika.
Ndugu zangu ninyi wote ni mashahidi kuwa zipo changamoto nyingi katika sekta ya elimu ndani ya nchi  yetu  zinazohusiana  moja kwa moja na masuala niliyoyataja hapo juu.Huku tukilenga kupata;
    •madawati 15,000,
    •matundu ya vyoo vya kisasa 1335,
    •visima vya maji 12, na
    •vyumba maalum vya watoto wa kike 38.

Kimsingi kampeni hii ni muendelezo wa kampeni iliyowahi kufanyika katika kata ya KIPAWA [ndani ya jimbo la Segerea] kwa kusimamiwa na mfuko wangu  wa elimu uitwao BONNAH  EDUCATION TRUST FUND   mnamo mwaka 2011,kipindi nilipokuwa diwani wa kata hiyo.Kwakuzingatia  mafanikio na matokeo chanya ya kampeni hii katika ngazi ya kata;


Kwa moyo wa dhati kabisa, kwakuwa  nimechaguliwa kuwa mbunge wa jimbo la Segerea ,nimedhamiria kupeleka mafanikio ya kampeni  hii kwa kushirikiana na mfuko wangu wa  BONNAH EDUCATION TRUST FUND katika ngazi ya jimbo ili basi kila mwananchi ndani ya jimbo la Segerea  anufaike na kampeni hii.
Ili kufanikisha kampeni hii, tutawashirikisha wadau mbalimbali wa elimu waliopo ndani na nje ya jimbo la Segerea kama vile Serikali, Makampuni, Mashirika na watu  binafsi.
  
Kampeni ya MAZINGIRA BORA KWA ELIMU BORA tunatarajia kuifanya kwa awamu mbili ambazo ni;
    ¡. Matembezi  ya  hiyari (Charity walk) na
   ¡¡. Chakula cha jioni (Gala dinner).

MATEMBEZI YA HIYARI.
Matembezi haya yatafanyika ndani ya jimbo kwa kushirikisha wananchi ,na wadau wote wa elimu tukiwa na lengo moja tu la kukusanya fedha za kuboresha miundombinu ya elimu katika jimbo letu la Segerea  kwa shule za msingi katika kata zote kumi na tatu[13] za jimbo la Segerea.
Matembezi haya yanatarajiwa kufanyika tarehe 25/02/2016, kuanzia saa 2 asubuhi mpaka saa 10 alasiri.

CHAKULA CHA JIONI
Awamu hii ya pili na ya mwisho ya kampeni yetu inatarajiwa kufanyika tarehe 03/06/2016 kuanzia  saa 2 usiku na kuendelea.
Katika awamu hii tunatarajia kuwa na chakula cha jioni cha pamoja ambapo wageni kutoka maeneo mbali mbali na nje ya nchi watashiriki nasi katika kuchangia na kuhamasisha upatikanaji wa fedha  na mahitaji yote muhimu kuelekea ufanikishaji wa kampeni yetu.

Tunawashukuru ninyi waandishi wa habari na wageni  wote waalikwa kwa kushiriki nasi katika uzinduzi huu wa kampeni  hii ya MAZINGIRA BORA KWA ELIMU BORA  jimbo la Segerea.

Hivyo natangaza  rasmi kuwa kampeni  hii imezinduliwa rasmi leo tarehe 17/01/2016.

Ahsanteni sana
Mawasiliano
Mh.Bonnah Kaluwa ; 0758 324  552
Bi. Jackline;   0713 711  632
Bw.Shamsudin; 0713 754 869



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.