STATE HOUSE
ZANZIBAR
OFFICE OF THE
PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 7.10.2017

SERIKALI ya Mapinduzi ya
Zanzibar hivi sasa imo katika hatua za kuendelea kukamilisha taratibu
zilizobaki ili kuanza ujenzi wa barabara ya Bububu-Kinyasini hadi Mkokotoni,
ujenzi ambao unatarajiwa kuanza hivi karibuni.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein,
aliyasema hayo katika hotuba yake wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa
kijiji cha Bandamaji, Mkoa wa Kaskazini Unguja, pamoja na waumini wa dini ya
Kislamu waliofika kijiji hapo kwa ajili ya ufunguzi wa msikiti wa Saeed Al Bawady, ambapo Dk. Shein alikuwa mgeni
rasmi.
Katika
hotuba yake hiyo, Dk. Shein alisema kuwa ndani ya kipindi cha wiki mbili
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inategemea kukamilisha hatua ya utiaji saini
wa mikataba na Wakandarasi.
Dk.
Shein alieleza kuwa hivi sasa tayari Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
imeshalipa fidia katika Shehia nyingi ambazo barabara hiyo inapita na imo
katika matayarisho ya kulipa wahusika katika Shehia 5 tu zilizobaki ambazo ni
Kinyasini, Chaani Masingini, Mkwajuni, Kivunge na Mkokotoni.
Aliongeza
kuwa matayarisho ya kulipa fidia kwa Shehia hizo zilizobakia yanakwenda vizuri
kwa lengo la kurahisisha ujenzi wa barabara hiyo muhimu.
Pamoja
na hayo, Dk. Shein aliwaeleza wananchi hao kuwa ujenzi wa barabara ya Bububu-Kinyasini
hadi Mkokotoni utaanzia huko maeneo ya Chuini, Wilaya ya Magharibi ‘A’, Mkoa wa
Mjini Magharibi.
Akiwa
katika ziara zake za kuitembelea Mikoa na Wilaya zote za Unguja na Pemba mnamo
mwezi wa Agosti mwaka huu, mara baada ya kuweka jiwe la jiwe la msingi katika
Mradi wa Soko la Kinyasini, Dk. Shein aliwaeleza wananchi wa Mkoa huo azma ya
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuijenga barabara hiyo ambapo kumalizika
kwake kutasaidia kiasi kikubwa kuimarisha sekta ya usafiri na usafirishaji kwa
wananchi wa Mkoa huo.
Kukamilika
kwa ujenzi huo kutawasaidia wananchi wa Mkoa huo wa Kaskazini Unguja pamoja na
mikoa jirani kupata kufaidika na huduma ya miundombinu bora ya barabara kwa
ajili ya usafiri sambamba na kuwasaidia katika shughuli zao za maendeleo
zikiwemo za kilimo, biashara pamoja na kuimarisha sekta ya utalii.
Sambamba
na hayo, katika hotuba yake hiyo, Dk. Shein alieleza kuwa Mkandarasi
atakaejenga barabara hiyo ndiye atakaejenga barabara tatu nyengine ambazo ni
barabara ya Matemwe hadi Muyuni, Pale Kiongele hadi Mkwajuni na Fuoni hadi
Kombeni.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment