Habari za Punde

Meli ya utafiti wa Mafuta na Gesi Asilia kupita karibu na mwambao wa kisiwa cha Pemba

                                       SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

         WIZARA YA HABARI UTAMADUNI UTALII NA MICHEZO


Tel: 0255 24 2237325/0255 24 223               7313                                 Idara ya Habari Maelezo
Fax: 0255 24 2237314                                                                            P.O.Box 2754
E-mail:habarimaelezo@yahoo.co.uk, maelezozanzibar@zanlink.com                Zanzibar
maelezozanzibar@hotmail.commaelezozanzibar@gmail.com                                                   

         

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Meli inayofanya utafiti wa Mafuta na Gesi Asilia ya MV. BGP EXPLORER ya China leo itakuwa katika maeneo ya karibu sana na Mwambao wa Kisiwa cha Pemba wakitokea Kusini Magharibi ya Kisiwa hicho.

Kwa saa 38 zijazo, Meli hiyo ya Utafiti wa Mafuta na Gesi Asilia kwa njia ya Mitetemo Baharini ikifanya utafiti eneo lote la Pwani ya Magharibi ya Kisiwa cha Pemba na hivyo Meli itakuwa ikitembea karibu sana na Kisiwa.

Hadi kufikia jana, Watafiti hao wametafiti njia 14 licha ya Mvua kubwa inayoendelea kunyesha ambapo pia wamekumbana na ukungu katika Pwani ya Kusini Magharibi ya Kisiwa cha Pemba.

Serikali inawaomba wananchi wasiwe na wasiwasi watakapoiona Meli hiyo ambayo kwa sasa itakuwa ikitembea karibu sana na Kisiwa.

Mamlaka ya Udhibiti wa Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta Zanzibar(ZPRA) inawaomba radhi Wavuvi kwa usumbufu unaojitokeza hasa pale wanapolazimika kusubiri kwa saa kadhaa kupisha shughuli za utafiti wakati Meli inapopita karibu na maeneo ya uvuvi.

ZPRA inawaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano katika zoezi hili na inawashukuru kwa ushirikiano wao wanaoutoa wakati wote wa zoezi la Mitetemo Baharini.

Imetolewa na :


Dk. Juma Mohammed Salum
K.N.Y
Mkurugenzi
Idara ya Habari(MAELEZO) Zanzibar
05, Novemba, 2017


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.