Habari za Punde

Wananchi wa Kijiji cha Kibele Zanzibar Wajumuika na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Shein Katika Iftar Aliyowaandalia Nyumbani Kwake Kibele Wilaya ya Kati Unguja.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akifuatana na Wanafamili wakati alipokuwa akielekea msikitini Nyumbani kwake Kibele Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja kabla ya  futari aliyoiandaa kwa Wananchi aliowaalika jana pamoja na familia yake
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akiwa katika futari na Viongozi aliowaalika pamoja na Wananchi mbali mbali Nyumbani kwake jana  Kibele Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja
Baadhi ya Viongozi na Wananchi mbali mbali wakiwa katika futari iliyoandaliwa  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein nyumbani kwake Kibele Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja jana
.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein (katikati), Waziri wa Biashara na Viwanda Mhe.Balozi Amina Salum Ali (kulia),Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe.Mgeni Hassan Juma(kushoto) akifuatiwa na Waziri wa Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji Mhe.Dk.Sira Ubwa Mamboya,wakiwa katika Futari iliyoandaliwa na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) nyumbani kwake Kibele Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja jana
 Baadhi ya Akinamama kutoka sehemu mbalimbali walioalikwa katika futari Nyumbani kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein, Kibele Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja jana
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) pamoja na Viongozi mbali mbali na Wananchi wakiitikia Dua Iliyoombwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi jana Baada ya Futari iliyofanyika Nyumbani kwa Rais, Kibele Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja jana
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akiagana na Viongozi mbali mbali na Wananchi  baada ya Futari iliyoiandaa na kuwaalika Nyumbani kwa Rais, Kibele Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja jana
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akiagana na Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Mhe.Simai Mohamed Said, baada ya Futari iliyoiandaa na kuwaalika mbali mbali Nyumbani kwake  Kibele Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja jana, [Picha na Ikulu.] 09/06/2018.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.