Habari za Punde

Salamu za UNFPA Siku ya Kuadhimisha Idadi ya Watu Duniani Celebration of World Population Day 2018 ‘’Family Planning is a Human Right’’

Mwakilishi Mkaazi wa UNFPA Tanzania Ms. Jacqueline Mahon, akitowa salimu za UNFPA katika Hafla ya Maadhimisho ya Siku ya Idadi ya Watu Duniani Zilizoadhimisha Kitaifa Zanzibar katika Ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.

Assalaam Alaykum;
Habari za Leo! Karibuni  sana kwenye Siku ya Idadi ya Watu Duniani
Ndugu Mgeni Rasmi, Wageni waalikwa, Mabibi na Mabwana,
Ninayofuraha kubwa kuwakaribisha  nyinyi nyote  katika maadhimisho haya ya siku ya Idadi ya Watu  Duniani 2018 yakiwa na kauli mbiu ya “Uzazi wa Mpango ni Haki ya Binaadamu”. Huu ni ujumbe mzuri kabisa ambao unaendana na hali halisi ya masuala ya Idadi ya watu katika nchi  mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania.
 Nchi wanachama wa Umoja wa mataifa, zilikubaliana kuwa  tarehe 11 July  kila mwaka iwe siku ya kuadhimisha siku ya Idadi ya Watu Duniani. Hii ni siku ambayo tunapaza sauti zetu  na kuelekeza nguvu juu ya umuhimu wa masuala ya Idadi ya Watu duniani. Kauli mbiu ya mwaka huu inavosema  Uzazi wa Mpango ni haki ya  Binaadamu”, inaendana moja kwa moja na masuala ya idadi ya watu na ajenda za kimaendeleo ya zama hizi pamoja na hali halisi katika nchi zetu. 
 Muhimu Zaidi ni kwamba Siku ya Idadi ya Watu Duniani inalenga kupinga dhana ya kwamba uzazi wa mpango ni kudhibiti Idadi ya Watu, baali ni kuhakikisha kuwa vizazi vyetu hawaichukulii haki hii kwa mzaha. Pia siku hii inalenga kuimarisha haki za kidunia na mfumo wa maendeleo ambao unaendana nao.
Ndugu Mgeni Rasmi, Wageni waalikwa, Mabibi na Mabwana,
Miaka 50 iliyopita Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za Binaadamu, ulipitisha tamko mjini Teheran la May 13 1968 lililosema…na hapa ninanukuu  “Wazazi wana haki ya msingi ya kuamua bila kushurutishwa na kwa umakini idadi na mpishano wa watoto wao”- mwisho wa kunukuu.  Wakitambulisha makubaliano yaliyofikiwa ujumbe ulioratibu mapatano ulitangaza kwamba wamekubaliana Familia kujipangia wenyewe na sio kupangiwa.
 Uzazi wa mpango ni haki ya Msingi  kwa wenza kuutumia, na sio  kwa ajili ya kudhibiti Idadi ya Watu. Siku ya Idadi ya Watu Duniani  mwaka huu 2018 imebeba ujumbe wa kuadhimisha makubaliano haya ya Kihistoria.  
Ndugu Mgeni Rasmi, Wageni waalikwa, Mabibi na Mabwana,
Faida zinazopatikana kupitia uzazi wa mpango ziko nyingi. Mojawapo nikuwa uzazi wa mpango huwezesha upatikanaji wa njia za uzazi wa mpango kwa wenza na kwa wanawake;  hivyo ni muhimu sana kwa ustawi wa mwanamke pamoja na kuimarisha Afya  na maendeleo yake na jamii inayomzunguka..
Faida nyengine ni kama ifuatavyo:-                            
·        Uzazi wa mpango ni njia bora zaidi kuliko njia nyengine zote za kufikia maendeleo ya dunia katika kupangilia hali ya familia kwa masuala ya uzazi.   Endapo Wanawake na vijana watakuwa na fursa ya kupanga idadi ya watoto, lini, na kwa mpangilio gani, basi wasichana wengi zaidi watabakia skuli kuendelea na masomo  na wanawake wengi wanaweza kuamua kuingia ama kubakia katika sekta ya uzalishaji: Na bila shaka hapo tutaiona familia nzima, jamii na nchi kwa jumla ikifaidika.
·        Kwa kila Dola moja inayotumiwa kwa ajili ya Uzazi wa Mpango Serikali inaweza kuokoa mpaka jumla ya Dola sita na hivyo kufanya uzazi wa mpango wa hiari moja ya uwekezaji bora Zaidi kufanya.
·        Pia kwa upande wa faida za kiuchumi na kijamii, upatikanaji wa uhakika wa huduma bora za Afya ya uzazi zinakisiwa kuzalisha faida ya Dola 120 kwa kila dola iliyowekezwa.
Ndugu Mgeni Rasmi, Wageni waalikwa, Mabibi na Mabwana,
·         Uzazi wa Mpango vile vile unaweza kusaidia nchi kufikia ‘demographic dividend’, - yaani ukuaji wa uchumi unaotokana na ongezeko la uzalishaji linalotokana na ongezeko la watu wanaoingia kwenye shughuli za kiuchumi na kupunguza utegemezi.
·        Vilevile Matumizi ya njia za uzazi wa mpango yanazuia zaidi ya theluthi moja ya vifo vyote vya uzazi duniani  kwa kuwaruhusu wanawake kuchelewesha au kupangilia uzazzi, kuepuka  mimba zisizohitajika na kuepusha utoaji mimba usio salama.
·        Ufikiaji kamilifu wa mahitaji ya huduma za kisasa za uzazi wa mpango  utapelekea kupungufu ya vifo   sabini na sita elfu (76,000)  vya uzazi kila mwaka pamoja nakupungua vifo  vipya vya uzazi  laki nne na themanini (480,000)
·        Kuweza kupanga na kuchelewesha uzazi ni muhimu sana kwa vijana baleghe chini ya miaka 18 ambao wako katika hatari kubwa ya vifo na maumivu  yatokanavyo na mimba za utotoni.
·        Kwa uande wa magonjwa ya kujamihiana: Kiwango kikubwa cha maambukizi ya magonjwa ya kujamihina  kipo kwa vijana wa umri  kati ya miaka 15 na 24. Hivyo Matumizi ya njia za uzazi wa mpango hasa Condom za kiume na za kike yanatoa kinga mbili kwa pamoja …yaani kinga dhidi ya mimba zisizohitajika na kinga dhidi ya magonjwa ya kujamiina.
  Kwa hivyo UNFPA ina hamasisha kuongezeka kwa uwekezaji wa Kitaifa kwenye  huduma za uzazi wa Mpango, kuwepo uhakika wa upatikanaji wa vifaa tiba, na kuunga mkono jitihada za kutanua wigo wa  njia za kisasa za uzazi wa mpango na kuimarisha ubora wa huduma.
Mkazo wetu ni katika upatikanaji wa taarifa na huduma kwa vijana baleghe na makundi mengine yaliyohatarini Zaidi.
Ndugu Mgeni Rasmi, Wageni waalikwa, Mabibi na Mabwana,
Kufikia maendeleo endelevu ya Dunia ifikapo mwaka 2030, itategemea sana ni kwa kiasi gani haki ya Afya ya uzazi kwa wanawake na Vijana itatimizwa. Kutimiza mahitaji yao ya Uzazi wa Mpango ni uwekezaji wenye faida kiujumla kuliko mwengine
Naomba nimalizie kwa kusema kuwa UNFPA itaendelea kushirikiana na Serikali na wadau wengine wa maendeleo kuhakikisha ‘’kuwa na Dunia ambayo kila ujauzito unathaminiwa, kila uzazi ni salama na kila malengo ya kijana yanafikiwa’’.
 Asanteni Sana kwa kunisikiliza

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.