Rais Dk. Shein
alikutana na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(TAKUKURU) Kamishna wa Polisi Diwani Athumani aliyefika Ikulu mjini Zanzibar
kujitambulisha kwa Rais.
Katika mazungumzo kati
yake na kiongozi huyo, Rais Dk. Shein alieleza umuhimu wa kuendeleza
mashirikiano kati ya (TAKUKURU) na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi
Zanzibar (ZAECA).
Rais Dk. Shein alieleza
kuwa licha ya taasisi hizo kwa kila moja kufanya kazi zake lakini bado zote
zina kazi ya kupambana na kudhibiti rushwa na kusisitiza kuwa kupambana na
rushwa na kusimamia maadili ya viongozi ni mambo ya msingi katika utawala bora
ambapo iwapo yakifanywa vizuri yatawasaidia wananchi.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Kamishna wa Polisi Diwani Athumani alieleza
kuwa suala la rushwa ni changamoto kubwa ambayo si kwa Tanzania tu bali ni
dunia nzima.
Alisema kuwa rushwa
inawagusa moja kwa moja wananchi wa kada zote hasa katika eneo la maendeleo
hivyo mashirikiano ya pamoja yanahitajika katika kupambana nayo.
Alisisitiza kuwa
kumekuwepo mashirikiano makubwa kati ya Taasisi hiyo na ile ya Zanzibar ambapo
miongoni mwa maeneo wanayoendelea kushirikiana ni pamoja na utoaji mafunzo na
kubadilishana uzoefu.
Rais Dk. John Pombe
Magufuli alimteua Kamishna wa Polisi Diwani Athumani kuwa Mkurugenzi Mkuu wa
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mnamo Septemba 6, 2018
ambapo anachukua nafasi ya Kamishna wa Polisi Valentino Mlowola ambaye
ameteuliwa kuwa Balozi.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment