WAZIRI wa Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar. Mh.Maudline Castico(wakwanza
kushoto) akikagua jengo lenye madarasa matatu ya kusomea
katika shehia ya Kipange Wilaya ya Micheweni.
WAZIRI wa Kazi Uwezeshaji Wazee,Wanawake na Watoto Zanzibar.Mh. Maudline Castico (wakwanza kulia) akizungumza na
wananchi ya shehia ya Kipange Wilaya ya Micheweni mara baada ya kukagua ujenzi
wa banda lenye madarasa matatu Skuli ya maandalizi Kipange.
Na Mwandishi wetu Pemba
WAZIRI wa Kazi Uwezeshaji
Wanawake na Watoto Mh.Maudline Castico amewataka wazazi kisiwani Pemba
kushirikiana na walimu katika kuhakikisha wanafunzi wanasoma vizuri na kufaulu.
Alisema hayo wakati
alipofika kukagua maendeleo ya ujenzi wa madarasa matatu ya maandalizi katika
kijiji cha Kipange Konde wilaya ya Micheweni.
Alisema, ufaulu wa wanafunzi
unakwenda sambamba na upatikanaji wa ushirikiano wa dhati kati ya wazazi na
walimu.
“Ili mtoto aweze kufanikiwa
vizuri kielimu hatuna budi kuwa sambamba na mwalimu, mwalimu ndiye anaefahamu
maendeleo ya mwanafunzi” alisema.
Sambamba na hilo aliwataka
wazazi hao kufuatilia kwa karibu nyendo za watoto ili kudhibiti mporomoko wa
maadili ikiwemo udhalilishaji wa watoto.
Aliongeza kuwa kutokana na
kuwepo kwa vitendo vya udhalilishaji ni vyema wazazi wakajenga mazoea ya
kuwafahamu watu ambao wanakua karibu na watoto wao ili kuchukua hatua mapema.
Aidha waziri Castico
aliwataka akina baba kuona wanawake wana daraja kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu
hivyo wanapaswa kuenziwa badala ya kuwanyanyasa.
Alisema bila ya msaada ,
nguvu na imani ya mwanamke wanaume wasingeweza kupata mafanikio waliyonayo sasa
hivyo ni lazima waoneshe shukurani kwao na kuwatunza na kuwapa heshima
inayostahiki.
Mapema wakisoma risala mbele
ya mgeni rasmi wazazi hao walieleza kuwa ujenzi wa madarasa hayo ulianza
mwishoni mwa mwaka 2017 kufuatia changamoto ya masafa kwa wanafunzi wa
maandalizi kutoka kijiji cha Kipange hadi mji wa Konde.
Walibainisha kuwa katika
msimu wa mvua za masika watoto wa kijiji hicho hupata shida kutokana na hali ya
barabara kujaa maji hali inayopelekea kushindwa kufika skuli mapema.
Walisema ujenzi huo ambao
unatokana na nguvu ya umoja wa wananchi wa kijiji hicho na serikali hadi
kufikia hatua ya kuezeka umegharimu jumla ya Tsh 4,870,500/=
Aidha waliishukuru Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi waMh. Rais Dk. Ali Mohamed Shein kwa
kuendelea kuboresha huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo elimu, maji na
barabara.
No comments:
Post a Comment