MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella katikati akikata utepe wakati wa
sherehe ya ufunguzi wa soko la madini ya vito wilayani Mkinga kulia ni
Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Tanga Zabibu Napacho kushoto ni Mkurugenzi
wa madini wa shirika la Pact Cristina Villegas akifuatiwa na Mwenyekiti
wa Chama cha Wanawake wachimba Madini Tanzania (Tawoma) Eunice Negelo
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza wakati wa uzinduzi
huo kulia Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Tanga Zabibu Napacho kushoto ni
Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake wachimba Madini Tanzania (Tawoma) Eunice Negelo
Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Tanga Zabibu Napacho akizungumza wakati
wa halfa hiyo kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella
akifuatiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake wachimba Madini Tanzania
(Tawoma) Eunice Negelo
Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake wachimba Madini Tanzania (Tawoma)
Eunice Negelo akizungumza kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine
Shigella kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Mkinga Mark Yona
Mkuu wa wilaya ya Mkinga Mark Yona akizungumza kulia Mwenyekiti wa
Chama cha Wanawake wachimba Madini Tanzania (Tawoma) Eunice Negelo
Mkurugenzi wa madini wa shirika la Pact Cristina Villegas akizungumza
wakati wa ufunguzi huo ambapo aliipongeza Serikali ya awamu ya tano
MENEJA wa (TRA) Mkoa wa Tanga Specioza Owure akizungumza wakati wa ufunguzi huo
Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake wachimba Madini Tanzania (Tawoma)
Eunice Negelo kushoto akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine
Shigella wakati wa ufunguzi wa soko la Madini wilayani Mkinga kulia ni
Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Tanga Zabibu Napacho kushoto ni Mkuu wa
wilaya ya Mkinga Mark Yonna
Sehemu ya wadau wa madini na wachimbaji wakiwa kwenye ufunguzi huo
Sehemu ya wadau wa madini na wachimbaji wakiwa kwenye ufunguzi huo
Sehemu ya wadau wa madini na wachimbaji wakiwa kwenye ufunguzi huo
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akionyeshwa aina ya madini
Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake wachimba Madini Tanzania (Tawoma)
Eunice Negelo katikati akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine
Shigella kulia na Mkuu wa wilaya ya Mkinga Mark Yonna kushoto na kulia
ni Katibu wa Tawoma Salma Kundi mara baada ya kufanya ufunguzi wa soko
la madini wilayani humo
Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake wachimba Madini Tanzania (Tawoma)
Eunice Negelo kushoto akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine
Shigella
Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake wachimba Madini Tanzania (Tawoma)
Eunice Negeloakiwa na Katibu wake kushoto Salma Kundi wakiteta jambo na
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kulia na anayefiuatia ni Mkuu wa
wilaya ya Mkinga Mark Yonna
Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake wachimba Madini Tanzania (Tawoma)
Eunice Negelo kushoto akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine
Shigella
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akiwa kwenye picha ya pamoja
mara baada ya sherehe ya ufunguzi wa soko la madini ya vito wilayani
Mkinga .
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella amesema Serikali itahakikisha inaendelea kuzipatia ufumbuzi wa kudumu changamoto zinazowakabili wachimbaji wadogo wadogo nchini ambazo zimekuwa ni kikwazo cha maendeleo yao.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigela
wakati wa sherehe ya ufunguzi wa soko la madini ya vito wilayani Mkinga .
Alisema kuwa licha ya wachimbaji hao kufanya kazi nzuri ya
uchmbaji lakini wamekuwa wakikabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo
uduni wa vifaa ,masoko pamoja na mitaji .
“Ufunguzi wa soko hili ni kielelezo cha kuonyesha namna
ambavyo serikali yenu ipo tayari katika kuanza kushughulikia changamoto
zenu kwani uwepo wa soko hili tayari ni mkombozi kwenu”alisema Mkuu wa
mkoa huyo.
Alisema kuwa changamoto nyingine ni namna ambavyo wataweza
kuongeza thamani madini hayo ili yaweze kupata soko la uhakika na kwa
haraka.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake wachimba Madini
Tanzania (Tawoma) Eunice Negelo alisema kuwa uwepo wa soko hilo
utasaidia kudhibiti
utoroshwaji wa madini.
Vile vile alisema kuwa uwepo wa soko hilo utaweza
kuwasaidia wachimbaji wadogo kupata fursa ya masoko ambapo hapo awali
ilikuwa ni changamoto kubwa kwao.
“Tunaimani sasa serikali itaweza kupata mapato yake vizuri
na wachimbaji wataweza kuuza madini yao kwa uhakika bila ya hofu ya
kuweza kutapeliwa na wajanja wachache”alisema Mwenyekiti huyo.
Hata hivyo Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Tanga Zabibu Napacho
alisema kuwa soko hilo ndilo ambalo litaweza kutoa dira ya uanzishaji wa
masoko mengine mkoani humo.
Alisema kuwa mkoa huo unautajiri wa madini lakini
wachimbaji wadogo waliowengi walikuwa hajaweza kunufaika biashara hiyo
kutokana na ukosefu wa masoko ya uhakika.
Mkurugenzi wa madini wa shirika la Pact Cristina Villegas
aliipongeza serikali kwa kuja na uamuzi wa masoko hayo kwani utasaidia
kuzui utoroshwaji wa madini kwa kiasi kikubwa.
“kwa uwamuzi wa serikali utasaidia kudhibiti mapato yake
lakini na mchimbaji mdogo ataweza kuona manufaa ya shughuli ya uchimbaji
anayoifanya’alisema Villegas.
No comments:
Post a Comment