Na MWANDISHI WETU
Agenda nyingi za Mabeberu wa
ndani na nje ya nchi hakika ni fursa ya
kipekee kwa Watanzania kujua jinsi ya kukabiliana nazo, kupambana nazo kwa njia
sahihi ambayo inawanufaisha na kutengeneza kipato kwa ajili ya maendeleo ya mtu
mmoja mmoja , familia na Taifa kwa ujumla.
Tanzania nchi huru iliyopata uhuru
wake tarehe 09 Desemba mwaka 1961 ina kila sababu ya kuona imekomaa kiasi gani
na kamwe sio nchi ya kubabaishwa na mabeberu wanaoimezea mate kila kukicha.
Mabeberu wanasahau kuwa Tanzania Taifa lililobarikiwa na Mwenyezi Mungu kwa
kuwa na Amani, Utulivu na Mshikamano wa watu wake kitu ambacho kinaonewa wivu
na mataifa ya ndani ya Bara la Afrika na duniani kote.
Tanzania kwa asili ni Taifa kiongozi wengine wanafuata katika masuala
mbalimbali ya kimataifa na taifa ambapo yanaanzia nyumbani, lakini upende
usipende yanahusisha dunia bila kutarajiwa na wale wanaoionea kijicho nchi
yetu. Tanzania imepewa heshima Duniani katika rpoti ya nchi zenye
Amani zaidi duniani mwaka 2020, Tanzania imetambulika kuwa moja ya nchi zenye
amani zaidi duniani huku ikishika nafasi ya kwanza kwa nchi za Afrika Mashariki
Wakati Mabeberu wa nchi wanapopanga
mbinu za kuiharibu, kuivuruga, kubomoa ustawi wa nchi yetu na kuiondoa Amani
tuliyonayo, ili wapate fursa ya kunyonya rasilimali zetu na kudhalilisha utu
wetu, Watanzania wako macho hawadanganyiki ila wanapata fursa ya kutafuta njia ya kuhimili
vishindo vyao kwa kuchapa kazi kwa
bidii, kujineemesha na kujinufaisha kwa rasilimali alizowajalia Mwenyezi Mungu .
Mfano hai ni wakati muafaka huu wa
uchaguzi wapo wanaotaka kujipenyeza kuhakikisha mwanya huu wa kufanya uchaguzi
unakuwa ndio wakati muafaka wa kubomoa Taifa la Tanzania lakini wamechelewa
badala yake ndio kwanza kila kukicha Watanzania wanamilila mola wao wapite
salama kwa amani na kuhakikisha Umoja, Utul;ivu na Mshikamano unawaumbua wale
wote wanaodhani ni wakati sahihi kujipenyeza.
Aidha, zama za ujima za kupewa
shanga, nguo na pesa na kuuza watu wetu, kuwadhalilisha na kuwapa viongozi wetu
matoi na vitu ambavyo havina thamani kama utu wa binadamu, umepitwa na wakati
kwa kuwa misingi iliyojengwa na waasisi wetu hayati Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere na Shekh Abeid Amani Karume imejengwa kwa zege la chuma ambalo
kulivunja haiwezekani.
Akihutubia Kongamano la Maombi
Maalum ya Dua na Sala kwa Ajili ya
Uchaguzi Mkuu 2020 lililofanyika Uwanja wa Jamhuri Mkoa wa Dodoma Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu
Nyerere, Joseph Butiku, amesema “ Tanzania ni nchi huru ambayo kila
Mtanzania anapaswa kujivunia kuwa yuko huru na ana haki ya kuheshimiwa utu wake
na utamaduni wa Watanzania daima utadumishwa hatutaki kuletewa mila na desturi
zinazoharibu umoja wetu”.
Mzee Butiku amesema “Maneno haya
matatu yakizingatiwa ya Amani, Umoja na
Maendeleo yetu wote yanayotokana na juhudi zetu sisi wenyewe.
Aidha, ameongeza na amesema “Kwa nini
nipo hapa katika umri huu wa miaka 82 ni kushirikiana na nyinyi wote na
Mheshimiwa Rais wetu nikiwa bado najisikia mwenye nguvu na kukumbushana kuhusu umuhimu
wa jambo hili Amani ya Taifa letu, Umoja
ya Taifa letu na Maendeleo ya Watanzania katika Taifa lao, umuhimu wa uongozi
bora wa Taifa letu na jinsi ya kupata uongozi na viongozi bora kupitia mchakato
wa uchaguzi ulio huru, haki na unaotoa matumaini” amesisitiza Mzee Butiku.
Nawakumbusha waasisi wa Taifa letu
Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Shekh Abeid Amani Karume tunakumbuka walivyohangaika kujitolea na
kuhatarisha maisha yao katika kuweka misingi, taratibu za uongozi wa nchi
wakitanguliza watu waliokuwepo wakati
huo na watakaokuja baadaye wakazingatia usawa wa watu hao, heshima ya watu hao,
demokrasia yao na haki zao wote bila
ubaguzi wowote. Misingi hiyo ya usawa bila ubaguzi wa aina yeyote heshima kwa
watu wote, haki sawa kwa watu wote, mbele ya sheria na katika fani za aina
mbalimbali na kutochanganya siasa na imani za dini zetu ndio iliyotujengea
Amani, Umoja, na maendeleo kwa watu wote.
Tukubali tukatae kama anavyosema Rais
wetu Dkt John Pombe Magufuli kuwa vita ya uchumi ni ngumu kwani inakuwa na
vikwazo vingi kutoka kwa mabeberu hawafurahii maendeleo ya Tanzania, Watanzania
muwe macho na watu wasioitakia mema Tanzania.
Mabeberu wamekuja na agenda zao na
kufanya hila mbalimbali za kuhujumu uchumi wakidhani wanawakomoa Watanzania
matokeo kuna mafanikio mengi sana ndani ya miaka mitano ambayo inaishangaza
dunia. Kwanza Tanzania kuingia Uchumi wa Kati kabla ya makusudio ya kufika
mwaka 2025 ni maajabu yaliyoiduwaza dunia hususan mabeberu wanaoimezea mate
nchi ya Tanzania.
Ushindi wa miradi mikubwa ya
kimkakati kama vile, reli ya kisasa (SGR), Bwawa la Umeme la Nyerere, ilikuwa
na pingamizi kutoka kwa bwana wakubwa wanaoshikilia dunia, Ufufuaji wa Shirika
la Ndege la Tanzania (ATCL) na ununuzi wa ndege 11, Usambazaji wa Umeme
Vijijini (REA), Ujenzi wa hospitali za Mkoa, Wilaya na uboreshaji na vituo vya
Afya na ujenzi wa vituo vipya ujenzi wa
miundombinu ya barabara kuunganisha
mikoa, wilaya na vijiji, Upanuzi wa Bandari zetu Bahari ya Hindi na Maziwa,
ununuzi wa meli mpya na vivuko vya kisasa
na ukamilishaji wa miradi ya maji
hakika ni maajabu mengine ambayo
mabeberu hawataki kusikia.
Hivi karibuni Tanzania imedhihirisha
haina utani na wahujumu uchumi kwa kuanzisha Mahakama ya Mafisadi na kuchukua
hatua mbalimbali kukabiliana nao ili kubadilisha mtazamo wa vizazi vijavyo kuwa
uhujumu uchumi ni kitu kibaya na sio utamaduni wa Mtanzania. Zaidi ya
watuhumiwa 467 wa uhujumu uchumi wamefikishwa kwenye vyombo vya sheria na kukiri makosa yao kwa kurejesha fedha za
umma bilioni 107 walizozifuja na mali kadhaa.
Aidha, zaidi ya magari 130 ambayo
yamefanya makosa mbalimbali hususan ya uhujumu uchumi, uhalifu wa dawa za
kulevya, ubebaji wa wahamiaji haramu na mengineyo yamesababisha magari hayo kutaifishwa na kupewa Serikali na Taasisi
za Umma zenye mahitaji ya magari kwa manufaa ya Watanzania.
Hivyo, majangili wa nyara za Serikali na wahujumu wa mali zetu za asili kama wanyama
pori, pembe za ndovu, madini, misitu (magogo) na samaki. Mabeberu wanaoiba
ubunifu wa Watanzania na kutangaza vitu vingi vya Tanzania kuwa ni vyao hakika
wameumbuka kwa kuwa sasa kila kilicho chetu tunakijua na tunakitangaza ni cha
Tanzania.
Pia, kuna makongamano, shangwe ya
vijana na majukwaa mengi yaliyofanyika katika kuwapa elimu makundi mbalimbali
kama vile vijana, wanawake, walemavu na wasanii kabla ya kuanza kampeni yamewapa
mwanga Watanzania wa kufanya biashara ndani ya makongamano na mikutano husika
na kuhakikisha wanaufaika kiuchumi, ambapo hili ni pigo kwa mabeberu ambao
wanafurahia wakiona wananchi wanakosa fursa za kufanya biashara na kusahau
kampeni zinaanza ndio watafanya biashara sana na kunufaika kiuchumi.
Mabeberu walidhani watatumia mwanya
na kisingizio kuhusu ugonjwa wa Homa
Kali ya Mapafu iletwayo na virusi vya Corona na kuhakikisha wanadhoofisha
uchumi na juhudi za Tanzania katika kuwaletea Watanzania maendeleo, lakini
Mungu amewaacha mabeberu hao midomo wazi kwani Tanzania ni salama zaidi na hakuna maambukizi ya Corona.
Kwa kuwa Dunia imefahamu jinsi Tanzania
ilivyopambana na ugonjwa wa Corona na
Shirika la Afya Duniani (WHO) kuaamua kufuata nyayo za Tanzania za kutowafungia watu ndani, kufungua shule,
vyuo vyote Barani Afrika na kuendelea kuchukua tahadhari japo ukweli ni kwamba hawataki
kumtanguliza Mungu ili awaepushe na
janga hilo.
Aidha, Taasisi ya Kimataifa
inayofanya Uchunguzi kwa Serikali za Afrika, Asia ndani na nje ya mabara yao
yenye Makao Makuu yake nchini Norway (Whisteblowers
Investigation Worldwide- WIW) imedhihirisha kuwa mabeberu wanaifatilia na
kuinyemelea Tanzania kwa kutumia hali na mali ilimradi ihakikishe inapenyeza agenda zao za kuendelea kuinyonya na
kuikandamiza Tanzania.
Kutokana na harakati mbalimbali za mabeberu
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(TAKUKURU) imepata fursa na imefanikiwa kuokoa fedha na mali zenye jumla
ya shilingi bilioni 273.38, na kutaifisha fedha taslim shilingi milioni 899
katika kipindi cha uongozi wa Serikali ya Awamu
ya Tano inayoongozwa na Dkt John Pombe Magufuli. Kutokana na taarifa
iliyopatikana kutoka kwenye taasisi hiyo imeweza kuokoa Dola za Marekani
1,191,651 na Euro, 4,301,399. Ikiwa ni
pamoja na kuokoa nyumba nane zenye thamani ya shilingi bilioni 11.6, magari matano yenye thamani ya shilingi
milioni 126 na viwanja vitano.
Pia, TAKUKURU wameokoa Dola za Marekani
milioni 55.8, Euro milioni 43, magari 75, nyumba 41, viwanja 47 na mashamba 13,
vyote hivyo ni fursa kwa Watanzania
kutumia rasilimali zilizorejeshwa
kuzalisha kwa wingi mazao, na kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
Mafanikio mengine ambayo ni fursa ni
kuongezeka kwa kasi ya utambuzi na urejeshaji serikalini wa mali na fedha
vilivyotokana na vitendo vya rushwa. Mengine yaliyofatiliwa na Taasisi hiyo ni
wakwepaji wa kodi na rushwa katika madini, ambapo sasa fursa lukuki
zimejitokeza kwa wachimbaji wadogo wa madini ambapo mabeberu wamepata pigo
lingine kwa Tanzania kuwa nchi ya kwanza duniani kuwa na madini Tanzanite yenye
uzito mkubwa kuliko nchi yeyote duniani kilo 9.5 na kuwavutia watalii kutoka
sehemu mbalmbali duniani kuja kujionea utajiri huo.
Kama hiyo haitoshi zaidi ya Watanzania wengi wamejiajiri katika
sekta ya uchimbaji wa Madini na kujipatia riziki zao za kila siku na kufurahia
rasilimali aliyowapa Mwenyezi Mungu.
Pia hatua mbalimbali zilizochukuliwa na
serikali katika kuhakikisha Madini yanawanufaisha Watanzania imeleta matokeo ya Kampuni ya Barrick Gold Minning kuanza kulipa fidia
ya kodi ya Dola ya Marekani milioni 300 hii ni safari ndefu ya kuwapiga kikumbo
mabeberu
Vita ya ufisadi imefanikiwa
kuwachambua vibaraka wa mabeberu wala rushwa katika utekelezaji wa miradi ya
maji, afya na katika vyama vya ushirika ikiwa ni pamoja na masoko ya mazao ya
kilimo (AMCOS), wakopeshaji wasiokuwa na leseni, ufuatiliaji wa mali za Serikali
zilizoporwa au kuchukuliwa bila kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu wote wapo
kitanzini hawana pa kupumulia NCHI HII
HAINA NAFASI KWA MABEBERU NA VIBARAKA WAO.
No comments:
Post a Comment