Habari za Punde

ZEC Yamtangaza Mwakilishi Mteule wa Jimbo la Tumbatu Zanzibar

 Na.Jaala Ali  ZEC.

Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imemtangaza rasmin Mgombea wa Uwakilishi kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Mhe. Haji Omar Kheir kuwa Muwakilishi mteule wa Jimbo la Tumbatu.

Msimamizi wa Uchaguzi ZEC Wilaya ya Kaskazini “A” Bi.Miza Pandu Ali akizungumza na Vyombo vya habari katika Ofisi za Tume ya Uchaguzi Zanzibar zilizoko Gamba amesema Tume imetoa Uamuzi wa Kumtangaza Mgombea huyo baada ya kuwa ni Mgombea pekee wa nafasi ya Uwakilishi kwa Jimbo la Tumbatu Zanzibar.

Msimamizi huyo alieleza kuwa Tume imefanya maamuzi kwa mujibu wa masharti ya Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar Nam. 4 ya 2018 kifungu cha 59(a)(b) ambacho kinamtaka msimamizi wa Uchaguzi kumtangaza Mgombea pekee katika Jimbo au Wadi.

Aidha, Tume imemtangaza Ndg.Othman Khamis Fumu kuwa Diwani Mteule wa Wadi ya Kipange na Ndg.Simai Vuai Khamis kuwa Diwani Mteule wa Wadi ya Kijini kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi.

Akizungumza kwa niaba ya wateule wenzake Mhe. Haji Omar Kheir alisema Wagombea wote katika jimbo la Tumbatu wameridhishwa na busara na hekima kwa Watendaji wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar katika kufanya maamuzi sahihi ya pingamizi na rufaa zilizowasilishwa.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari juu ya uamuzi wa Rufaa iliyotolewa na Tume ya Uchaguzi ilimuengua Ndg.Haji Ali Haji Mgombea wa nafasi ya uwakikishi Jimbo la Tumbatu Zanzibar , Zuli Juma Simba       Wadi ya Kijini na Salum Khamis Maliki Wadi ya Kipange wote kwa tiketi ya ACT Wazalendo baada ya kushindwa kutimiza vigezo vya uteuzi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.