Habari za Punde

Rais Dk Hussein Ali Mwinyi awateua Nassor Mazrui na Omar Said Shaaban kuwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi


 STATE HOUSE ZANZIBAR

OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE

  Zanzibar                                             07.12.2020

---

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewateua Nassor Ahmed Mazrui na Omar Said Shaaban.

 

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, ilieleza kwamba uteuzi huo umeanza leo tarehe 7 Disemba, 2020.

 

Aidha, taarifa hiyo ilieleza kwamba kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu Namba 66 cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi amewateua viongozi hao kuwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.

 

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 

 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.