Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharib Idrissa Kitwana Mustafa akizungumza na Waandishi wa Habari katika mafunzo ya kushajihisha masuala ya Amani, Utangamano na Utamaduni wa kupokea maoni mbadala baada ya Uchaguzi Mkuu, (kushoto) ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Zanzibar Abdallah Mfaume. hafla iliyofanyika Ukumbi wa Kitengo cha Uzazi shirikishi Kidongo Chekundu Unguja.
Na Maryam
Kidiko / Mwashungi Tahir -
Maelezo. 23/12/2020.
|
Ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya waandishi wa habari juu ya kushajiisha masuala ya amani,utangamano na utamaduni wa kupokea maoni mbadala baada ya uchaguzi mkuu huko Ukumbi wa Kitengo cha Uzazi Shirikishi,Kidongo Chekundu Unguja.
Alisema
kuficha taarifa na kutoeleza ukweli kwa jamii hupelekea kuwepo uvumi na kujenga
dhana potofu na kutokuwa na imani kwa viongozi wao.
Aidha alisema
wananchi wanahitaji kupata taarifa zilizosahihi za matukio yanayotokea sehemu
mbali mbali ya maendeleo, kiuchumi na kisiasa kwa lengo la kuleta ufanisi na
kuendelea kuwa na amani nchini.
Mkuu wa Mkoa
huyo amewataka waandshi kufahamu mafanikio, maendeleo na ujenzi wa amani ya
taifa lolote duniani yanahitaji zaidi utolewaji wa taarifa kupitia vyombo vya
habari bila ya kutoka nje ya maadili ya kazi.
Hata hivyo
amewataka watendaji wa vyombo hivyo kutochoka kuibua vikwazo vinavyowakabili
wananchi na kuvifanyia kazi pamoja na kuyasemea yanayotekelezwa na serikali ili
wananchi kuyafahamu.
Akiwasilisha
mada katika mafunzo hayo, Mwandishi Mwandamizi Ali Sultan alisisitiza waandishi
kuacha ushabiki wa mambo yasiyo na faida kwa jamii pamoja na kuvilinda vyanzo
vyao vya habari ili kuepuka kuvunja amani katika fani hiyo.
Mafunzo hayo
ya siku mbili yameandaliwa na klabu ya waandishi wa habari zanzibar zpc kwa
ufadhili wa Internews.
No comments:
Post a Comment